Monday, January 24, 2011

Basi latekwa abiria wakatwa mapanga

IMERIPOTIWA kuwa watu wanane wamejeruhiwa vibaya na kulazwa katika hospitali ya Mkoa wa Singida baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka Kampala nchini Uganda kwenda Dar es Salaam kutekwa na majambazi na kisha kuporwa fedha pamoja na mali nyingine.

Basi hilo mali ya Kampuni ya Falcon Excutive lenye namba za usajili T.386 AUD aina ya Nissan. Licha ya abiria kuporwa mali anuai na fedha taslimu, pia wamekatwa kwa mapanga na kupigwa kwa mawe sehemu mbalimbali za miili yao. Robo tatu ya abiria hao walikuwa ni raia kutoka nchi ya Uganda.

Hata hivyo Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa,Rajabu Muhuwila, aalisema kuwa tukio hilo limetokea jana kati ya saa tano na sita usiku katika eneo la mlima wa Sekenke uliopo kata ya Shelui wilayani Iramba.


Alisema abiria hapo akiwemo hilo aitwae Omari Mzee, wameumizwa na hali ya dereva huyo imeleezwa kuwa ni mbaya alikuwa hajitambui. ..........Taarifa kwa Hisani ya Mdau Iramba.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...