Friday, October 28, 2016

Bi. Khadija Kopa Afunika Usiku wa Mshike Mshike Mwanza





Malikia wa Taarabu Afrika Mashariki na Kati, Khadija Omar Kopa, akitoa burudani kwa wakazi wa Jiji la Mwanza usiku wa kuamkia leo ndani ya Villa Park Resort kwenye show ya Usiku wa Mshike Mshike iliyoandaliwa na 102.5 Lake Fm Mwanza.




Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.




Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.





Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.




Wananzengo wakifurahia burudani iliyotolewa kwenye Usiku wa Mshike Mshike na 102.5 Lake Fm





Timu ya Uongozi na Wafanyakazi wa 102.5 Lake Fm Mwanza pia ilitambulishwa kwa Wananzengo kwenye show hiyo




Timu ya Uongozi na Wafanyakazi wa 102.5 Lake Fm Mwanza pia ilitambulishwa kwa Wananzengo kwenye show hiyo





Wananzengo kutoka 102.5 Lake Fm Mwanza




Timu ya Uongozi na Wafanyakazi wa 102.5 Lake Fm Mwanza pia ikijitambulisha kwa Wananzengo kwenye show hiyo




Madjz wa 102.5 Lake Fm, Dj Hcue (katikati), Dj KFlip (kushoto) na Dj Dhifa (kulia)




Dj Dhifa




Dj KFlip (kushoto) na Dj Hcue




Khadija Omar Kopa akihojiwa na wanahabari baada ya show




Hakika 102.5 Lake Fm Mwanza ni Raha ya Rock City na ni Redio ya Wananzengo. Kaa tayari kwa show ijayo.

TTCL, HUAWEI Wazinduwa Huduma ya Teknolojia ya 4.5G

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora (katikati) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi rasmi  wa matumizi ya teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano. Kulia ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Bw. Waziri Waziri Kindamba na Mkurugenzi Mkuu wa Huawei Tanzania, Bruth Zhang (kushoto) wakishuhudia.


Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora (katikati) akipiga makofi pamoja na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Bw. Waziri Waziri Kindamba (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Huawei Tanzania, Bruth Zhang (kushoto) mara baada ya uzinduzi wa matumizi ya teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano. 

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Bw. Waziri Waziri Kindamba akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa matumizi ya teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano. Hafla hiyo ilifanyika jana katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora akizungumza kabla ya kuzinduwa rasmi wa matumizi ya teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano. Hafla hiyo ilifanyika jana katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.



Afisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Peter Ngota akizungumza katika uzinduzi wa teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano. Hafla hiyo ilifanyika jana katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Huawei Tanzania, Bruth Zhang akizungumza katika uzinduzi wa teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni hiyo ambayo ni mshirika wa Kampuni ya TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano. Hafla hiyo ilifanyika jana katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.


Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora (mwenye suti ya kijivu) akizunguka kupata maelezo namna teknolojia ya 4.5G inayofanya kazi wengine ni viongozi waandamizi wa Kampuni ya Huawei na TTCL. Hafla hiyo ilifanyika jana katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora (mwenye suti ya kijivu) akizunguka kupata maelezo namna teknolojia ya 4.5G inayofanya kazi wengine ni viongozi waandamizi wa Kampuni ya Huawei na TTCL. Hafla hiyo ilifanyika jana katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora (mwenye suti ya kijivu) akizunguka kupata maelezo namna teknolojia ya 4.5G inayofanya kazi wengine ni viongozi waandamizi wa Kampuni ya Huawei na TTCL. Kushoto ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Bw. Waziri Waziri Kindamba.






Meza kuu ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora (mwenye suti ya kijivu) ikipata maelezo namna teknolojia ya 4.5G inayofanya kazi wengine ni viongozi waandamizi wa Kampuni ya Huawei na TTCL. 

Kulia mmoja wa wageni waalikwa katika hafla ya uzinduzi wa matumizi ya teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano akicheza gemu kwa kutumia teknolojia hiyo.

Afisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Peter Ngota (kulia) akipongezwa na baadhi ya wageni waalikwa mara baada ya kampuni ya TTCL kwa kushirikiana na Huawei kuzinduwa teknolojia ya 4.5G jana katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.






Sunday, October 23, 2016

Duka jipya la mavazi ya maharusi lafanya maonesho ya mavazi ya harusi


Mkurugenzi Mtendaji wa jarida maarufu nchini la Bang 'Bang Magazine', Emelda Mwamanga (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka jipya kubwa la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni mmiliki wa duka hilo, Mary Monyo pamoja na Mwendeshaji wa duka la Precious Wedding House, Victoria Chuwa (kulia). Uzinduzi huo uliofanyika Sinza Madukani ulikwenda sambamba na maonesha ya mavazi mbalimbali ya maharusi yaliofanywa na wabunifu wa mitindo maarufu kutoka Tanzania na Nigeria na wanamitindo chipukizi toka Tanzania. 

Mmiliki wa duka jipya kubwa la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaam jana, Mary Monyo (kulia) akimlisha keki Mkurugenzi Mtendaji wa jarida maarufu nchini la Bang 'Bang Magazine', Emelda Mwamanga (kushoto) wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliofanyika Sinza Madukani sambamba na maonesha ya mavazi mbalimbali ya maharusi yaliofanywa na wabunifu wa mitindo maarufu kutoka Tanzania na Nigeria. 
WABUNIFU wa mitindo maarufu kutoka Tanzania na Nigeria na wanamitindo chipukizi wamejitokeza kufanya maonesha ya mavazi mbalimbali ya maharusi katika uzinduzi wa duka jipya kubwa la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaa. Uzinduzi huo uliofanyika jana eneo la Sinza Madukani ulipambwa na mbunifu wa mitindo kutoka nchini Nigeria ajulikanaye kwa jina la Femi, mbunifu maarufu nchini Tanzania, Strayton Mashulano pamoja na baadhi ya wanamitindo chipukizi kutokea nchini Tanzania.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mwendeshaji wa duka la Precious Wedding House, Victoria Chuwa ambao ni waandaaji wa onesho alisema waliamua kufanya onesho hilo ili kutoa fursa kwa wananchi hasa wanaoelekea kufanya harusi kujua mitindo mbalimbali ya mavazi ambayo wanaweza wakaitumia katika shughuli zao za harusi na kuonekana tofauti kimuonekano.

Alisema wabunifu walifanya maonesho ya mavazi katika mitindo mbalimbali kutumia mavazi ya hali zote ikiwa ni kuonesha jamii harusi si lazima muhusika au maharusi kutumia gharama kubwa bali wanaweza kutumia gharama za chini na kuonekana wenye mvuto kama watapata ushauri kutoka kwa wabunifu na wanamitindo.


Mkurugenzi Mtendaji wa jarida maarufu nchini la Bang 'Bang Magazine', Emelda Mwamanga (kushoto) akimlisha keki Mmiliki wa duka la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaam jana, Mary Monyo (kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliofanyika Sinza Madukani sambamba na maonesha ya mavazi mbalimbali ya maharusi yaliofanywa na wabunifu wa mitindo maarufu kutoka Tanzania na Nigeria. 

Mmiliki wa duka la Precious Wedding House, Mary Monyo (kushoto) akimlisha keki Mwendeshaji wa duka hilo, Victoria Chuwa (kulia) mara baada ya uzinduzi wa duka la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaam. 

Mmiliki wa duka la Precious Wedding House, Mary Monyo (kushoto) akimlisha keki mmoja wa wageni waalikwa mara baada ya uzinduzi wa duka la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaam. 


Mbunifu maarufu wa mitindo kutoka nchini Nigeria, Femi (wa pili kushoto), pamoja na mbunifu maarufu nchini Tanzania, Strayton Mashulano (wa kwanza kulia) wakiwa katika pozi pamoja na baadhi ya wanamitindo chipukizi kutokea nchini Tanzania, kwenye maonesha ya mavazi mbalimbali ya maharusi yaliofanyika katika duka la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaam. 
Alisema duka lao pamoja na kuuza nguo za maharusi watakuwa wakitoa ushauri bure kwa maharusi endapo watafika katika duka hilo ambalo limekuja kuleta mabadiliko katika mitindo ya maharusi. Alisema duka hilo litahudumia watu wenye kipato cha chini, cha kati na hata cha juu kulingana na mahitaji ya wahusika huku wakinufaika kwa ushauri bure kila atakaetembelea na kuomba ushauri kwa wataalamu wa mitindo.

Alisema duka hilo kubwa la mitindo ya maharusi wa kike na kiume linatumia wataalamu wa mitindo kutoka nchi za Uturuki, Marekani, Italia pamoja na Tanzania. Alisema wamekuja kuondoa dhana iliyojengeka kuwa nguo za maharusi ni anasa kutoka na maduka mengi kuuza bei kubwa kuliko inavyotegemewa, hivyo kupitia kwa wataalam wao maharusi wanaweza kufanya shughuli kwa bei ndogo na kuvutia.

"...Watu wengi wanaona mavazi ya maharusi ni kama anasa kutokana na bei kubwa za mavazi haya, sisi tumeamua kuleta mabadiliko hapa dukani kuna nguo za makundi yote, yaani watu wa kipato cha chini, watu wa kipato cha kati na hata watu wa kipato cha juu...unaweza kuandaliwa nguo yako ya harusi na wanamitindo kutoka nchi tulizotaja wewe ukiwa hapa hapa nchini na ukaipata ndani ya siku 21.

Akizinduwa duka hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa jarida maarufu nchini la Bang, Emelda Mwamanga alimpongeza mwanamama mjasiliamali na mmiliki wa duka hilo, Mary Monyo kwa uamuzi wa kusaidia kutoa ushauri kwa maharusi jambo ambalo limekuwa likipasua vichwa kwa wahusika. Alisema kitendo hicho kinatoa changamoto kwa akinamama wajasiliamali kuweza kufanya mambo
makubwa kibiashara.

Mmiliki wa duka la Precious Wedding House, Mary Monyo akimkabidhi zawadi ya keki Mtangazaji wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani kupitia Times FM, Khadija Shaibu 'Dida' kwenye uzinduzi wa duka jipya kubwa la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo ulienda sambamba na siku ya kuzaliwa Khadija Shaibu 'Dida'.

Mmiliki wa duka la Precious Wedding House, Mary Monyo (kushoto) akimwonesha moja ya magauni ya maharusi Mkurugenzi Mtendaji wa jarida maarufu nchini la Bang 'Bang Magazine', Emelda Mwamanga (kulia) mara baada ya uzinduzi wa duka la mavazi ya maharusi 'Precious Wedding House' lililozinduliwa jijini Dar es Salaam jana. Uzinduzi huo uliofanyika Sinza Madukani ulikwenda sambamba na maonesha ya mavazi mbalimbali ya maharusi yaliofanywa na wabunifu wa mitindo maarufu kutoka Tanzania na Nigeria na wanamitindo chipukizi toka Tanzania. 

Mkurugenzi Mtendaji wa jarida maarufu nchini la Bang 'Bang Magazine', Emelda Mwamanga (kushoto) pamoja na Mtangazaji wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani kupitia Times FM, Khadija Shaibu 'Dida' wakifungua mvinyo kwenye  Uzinduzi huo uliofanyika Sinza Madukani.

Mmiliki wa duka la Precious Wedding House, Mary Monyo (kulia) akigonganisha glasi ya mvinyo na baadhi ya wageni waalikwa kwenye uzinduzi huo.

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...