Monday, August 10, 2020

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad

Seif Shariff Hamad


KWA
mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amekiri hadharani kuwa amezeeka na kwamba yeye sasa ni Babu huku akimtaja Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi kuwa ni kijana mwenye nguvu. 

Akihutubia wafuasi wake katika Ofisi za ACT-Wazalendo, Vuga mara baada ya mapokezi ya wagombea wao, Seif Shariff Hama amesema “Pole Pole anasema kuwa mimi ni Babu, ati kizee! ni kweli nakubali kuwa mimi ni babu na wao mgombea wao  Dkt. Hussein ni kijana, sasa nataka kuwauliza wajukuu zangu leo mtanichagua mimi babu au kijana?” Aliwauliza wafuasi wake ambao wengi walibaki na midomo wazi. 

Mgombea huyo wa Urais Zanzibar kupitia ACT-Wazalendo, katika hali ya  kukata tamaa alieleza kuwa yeye akiwa Babu licha ya umri wake kuwa mkubwa lakini atamshinda Mgombea Kijana wa CCM jambo ambalo liliwafanya wafuasi wake kuanza kuguna chini kwa chini huku akiwatuliza kwa kuwataka wasiwe na wasi wasi na uzee wake. 

Ifikapo Oktoba mwaka huu, Babu Seif Shariff Hamad atakuwa na umri wa miaka 78. Itakumbukwa kuwa Seif Shariff Hamad ni mgombea pekee aliyegombea mara nyingi  zaidi bila kushinda.

Alianza akiwa CCM Mwaka 1985 akashindwa na Sheikh Idriss –Abdulwakil, akaanza visa na vituko vya kuhujumu CCM ambapo Mwaka 1988 yeye na wenzake saba walifukuzwa Uanachama wa CCM. 

Mwana 1995 (uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi) aligombea na Dkt. Salmin Amour akashindwa. Mwaka 2000 aligombea na Amani Abeid Karume akashindwa. Mwaka 2005 aligombea tena na Karume akashindwa. Mwaka 2010 aligombea na Rais wa sasa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, Maalim Seif akaangukia pua.

Mwaka 2015 Maalim Seif aligombea tena na kushindwa. Mwaka 2020 anagombea na kijana Dkt. Hussein Mwinyi, na CCM wana uhakika wa  kumshinda 'asubuhi.' 

Hata mabango ya wafuasi wake pamoja na viongozi wenzake waliandika na kutamka maneno ya "Shikamoo Babu Seif"

Thursday, June 7, 2018

WAZIRI MKUU AWATAKA WABUNGE KUDUMISHA MSHIKAMANO

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Wabunge, baada ya futari aliyowaandalia, katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 5. 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasisitiza wabunge waendelee kudumisha  mshikamano ili Tanzania iendelee kuwa nchi tulivu na yenye amani.

Amesema mshikamano na upendo walionao wabunge hao ni vema wakauendeleza ili waweze kutekeleza shughuli zao za kuishauri Serikali.

Waziri Mkuu aliyasema hayo Juni 5, 2018 katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma wakati wa futari aliyowaandalia wabunge. Futari hiyo ilihudhuriwa na wabunge wa vyama vyote.

"Mshikamano na upendo huu tuliouonesha kuanzia mwanzo wa mkutano wa Bunge naomba tuudumishe ili tuweze kuishauri vizuri Serikali na tufikie malengo tuliyojiwekea,” alisema. 

Naye,Spika wa Bunge, Job Ndugai ambaye alitoa neno   la shukurani kwa niaba ya wabunge wote alimshukuru Waziri Mkuu kwa heshima aliyowapa.

"Tunakushukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, hii heshima uliyotupa ni kubwa, kualikwa na wewe si jambo dogo si kila mtu anaweza kupata nafasi hii," alisema.

Kwa upande wake, Mbunge wa Mgogoni, Mheshimiwa Dkt. Suleiman Ally Yussuf ambaye alisoma dua alisema watu wanatakiwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa uhai aliowapa.

“Kuna wenzetu tulioshirikiana nao kwenye mfungo wa Ramadhani mwaka uliopita lakini leo hatunao sababu wametangulia mbele ya haki, hivyo sisi tunatakiwa tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa uhai aliotupa,” alisisitiza.

Wednesday, June 6, 2018

Profesa Mbarawa akagua maendeleo ujenzi wa Tazara Fly Over

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida (kulia) wakikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya juu (Tazara Fly Over) leo jijini Dar es Salaam. Ujenzi huo kwa sasa umekamilika kwa asilimia 88.

Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida akijadiliana jambo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kulia) mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya juu (Tazara Fly Over) leo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (kulia) na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida (kushoto) wakijadiliana jambo mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya juu (Tazara Fly Over) leo jijini Dar es Salaam. 

Muonekano wa juu wa Barabara ya Nyerere eneo la Tazara (Tazara Fly Over) ambao kwa sasa ujenzi wake umekamilika kwas asilimia 88.


Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (Tanroards) Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Julius Ndyamukama akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida walipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya juu (Tazara Fly Over) leo jijini Dar es Salaam. 

Thursday, May 31, 2018

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AZINDUA WIKI YA MAZIWA NCHINI, AAHIDI KUINUA SEKTA HIYO


Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina(wa pili kulia) akikata utepe kuzindua Wiki ya Maziwa kitaifa kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro,kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na viongozi wa Baraza la Kilimo nchini na Bodi ya Maziwa.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina akitoa hotuba yake kwenye uzinduzi wa  Wiki ya Maziwa kitaifa kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro jijini Arusha.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina akiwapa wanafunzi wa Shule ya Msingi Baraa ya jijini Arusha  baada ya kuzindua Wiki ya Maziwa kitaifa kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro,kulia kwake ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo.

Meneja wa kampuni ya Milkcom maafuru Dar Fresh,Tunnu Mssika akimpa maelezo Waziri wa Mifugo na Uvuvi wakati akikagua mabanda ya waoneshaji bidhaa mbalimbali zinazotokana na mifugo.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina(katikati) akipewa maelezo na Mjasiriamali wa kampuni ya Mpilika Leather kutoka Dodoma,Anna Malongo ,kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo .

Wananchi waliohudhuria maadhimisho ya Wiki ya Maziwa kitaifa mkoa wa Arusha wakifatilia kwa makini hotuba za viongozi.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhaga Mpina(kushoto) akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Baraza la Wakulima nchini(ACT),Dk Sinare Sinare(kulia)kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro,wa pili kulia ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Maziwa,Lucas Malunde.

Monday, May 28, 2018

AMREF YAISHUKURU SERIKALI KUAMINI UTENDAJI WAO


 Mkurugenzi wa Amref Tanzania, Florence Temu (aliyekaa kushoto), akisaini mkataba wa kufanya kazi pamoja na Tayoa. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tayoa, Peter Masika. Anayeshuhudia katikati ni Mkurugenzi wa Bodi ya Uratibu ya Miradi ya Ukimwi, Malaria na Kifua Kikuu inayofadhiliwa na mfuko wa dunia Dr. Rachae Makunde.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Health Promotion Services (THPS), Redemputa Mbatia, akipeana mkono na Mkurugenzi wa Amref Tanzania, Florence Temu baada ya kusaini mkataba huo.

 Wadau wa masuala ya Afya wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Faustine Ndugulile, akihutubia kwenye uzinduzi huo.

 Emiliani Busara kutoka MDH, akizungumza kwenye uzinduzi huo.


 Mchungaji Basilisa Ndonde akizungumza kwenye uzinduzi huo.


 Mkurugenzi wa Amref Tanzania, Florence Temu (aliyekaa kushoto), akisaini mkataba wa kufanya kazi pamoja na MDH. Kulia ni Emiliani Busara kutoka MDH.

 Mkurugenzi wa Amref Tanzania, Florence Temu, akihutubia kwenye uzinduzi huo.

  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Faustine Ndugulile (wa pili kushoto), akiwa na viongozi wengine katika uzinduzi huo.

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tayoa, Peter Masika (kulia), akipeana mkono na Mkurugenzi wa Amref Tanzania, Florence Temu baada ya kusaini mkataba huo.

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tayoa,, Peter Masika, akihutubia.


 Mkurugenzi wa Bodi ya Uratibu ya Miradi ya Ukimwi, Malaria na Kifua Kikuu inayofadhiliwa na mfuko wa dunia Dr. Rachae Makunde ,  akizungumza kwenye uzinduzi huo.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mkapa Foundition, Rahel Sheiza (kulia),  akipeana mkono na Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florence Temu baada ya kuisaini makubaliano ya kufanya kazi pamoja.


Na Dotto Mwaibale

MKURUGENZI Mkazi wa Amref nchini Tanzania, Florence Temu ameishukuru serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli na zilizopita kwa ushirikiano inayotoa kwao.

Temu alitoa shukurani hizo kwenye uzinduzi wa mradi wa Amref Health Africa wa kupambana na Ukimwi na Kifua Kikuu unaofadhiliwa na Mfuko wa Dunia (Global Fund) uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Kwenye uzinduzi huo ambao mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee na Watoto, Dr.  Faustine Ndugulile walihudhuria pia Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri  wa Amref Tanzania, Dr. Eric Van Praag, Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linalojishughulisha na Ukimwi (UNAIDS), Dr. Leo Zekeng  na viongozi na wawakilishi wa mashirika mbalimbali  yaliyopewa dhamana ya kusimamia mpango wa mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi ili kufikia asilimia 90 ya  waishiyo na   VVU kupatiwa tiba na asilimia 90 ya walio kwenye tiba za VVU 90 wafanikiwe kufubaza VVU.

Temu alisema kuwa, baada ya kupitia michakato ya kutambua asasi itakayochukua jukumu la 'Principle Recipient' katika mkondo wa taasisi zisizokuwa za serikali, mwanzoni mwa mwaka jana, Amref Health Africa Tanzania ilihidhinishwa rasmi na hatimaye Februari 21 walisaini kama Principle Recipient wa mkondo wa taasisi zisizo za serikali Mfuko wa Dunia wa Fedha zenye thamani ya Bilioni 55 na milioni 256 na laki 7 (yaani $24,969,174) kwa ajili ya kuibua na kutibia VVU na Kifua Kikuu, wakikabidhiwa jukumu la kusimamia na kuratibu afua za kwenye jamii zihusuzo Ukimwi na Kifua Kikuu kwa kupitia asasi ya kijamii, takriban asilimia 10% ya fedha hizo zitaelekezwa katika afua za kukabiliana na Kifua Kikuu katika jamii.

Aliongeza kuwa, kwenye mapambano ya maradhi hayo wataifikia mikoa 15 ambayo ni Arusha, Dodoma, Kilimanjaro, Manyara, Mara, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Mwanza, Pwani, Shinyanga, Simiyu, Singida,Tanga na Ruvuma.

"Tunatarajia kupitia mfuko huu jumla ya watu 546,880 watafikiwa na huduma ya kupima VVU na kujua majibu, pia wasichana wa umri rika/ balehe na wanawake 162,064. Lakini pia kuibua na kuwapa rufaa wenye maambukizi ya kifua kikuu wapatao 16,465 watapata uchambuzi zaidi kwenye uwakilishi utakaofuata," alisema Temu.

Aliongeza kuwa, Amref inathamini kwa dhati jukumu walilopewa la kuratibu na kuongoza mradi huo uliofadhiliwa na Global Fund kwa miaka mitatu ijayo na kuahidi kufuata muongozo stahiki uliopo katika kutekeleza mradi huo, kwa dhana hiyo wanaahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na wadau husika kadiri watakavyoweza.

"Tutashirikiana moja kwa moja kama Amref lakini pia kwa kuwatumia sub recipients wetu ambao ningependa muwatambue," alisema Temu na kuwataja kuwa ni Tanzania Health Promotion Services (THPS), Management and Development fo Health (MDH), Benjamin Mkapa Foundition (BMF) na Tanzania Youth Alliance (TAYOA).
Aliongeza kuwa, wanatambua changamoto zilizopo katika kufikia jamii  hasa kwenye malengo ya kuwafikia wanaopaswa kujua hali yao ya maambukizi, ambapo kulingana na takwimu za Tanzania HIV Impact Survey ambao ni asilimia 52.2% ya walio na umri wa miaka 15-64 tu ndiyo wamepima na kujua hali zao za maambukizi; na uhaba wa wanaume kufikia huduma hizo, pia kuwepo kwa makundi yenye mazingira hatarishi zaidi ya kuambukizwa na kuambukiza VVU, pia haja ya kuibua wenye kifua kikuu na kuhudumia wenye TB sugu katika jamii, hizo ni baadhi tu!

Temu alisema wanatambua juhudi za Serikali ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha anafikia asilimia hizo 90 tatu na nia ya kutokomeza kifua kikuu na kudhibiti maambukizi na kupeleka huduma hizo katika ngazi za jamii kuimarisha mifumo ya usambazi dawa na vifaa tiba, kusomesha wataalam, kuboresha vituo vya afya na hospitali na mifumo ya rufaa ni juhudi za wazi na wanaipongeza wizara ya afya inayoongozwa na Waziri Ummy Mwalimu akishirikiana kwa karibu na naibu wake Dr. Faustine Ndugulile.

"Mfano nichomekee kidogo hapo jinsi Amref kwa kupitia brand ya Angaza tulivyoweza kuleta huduma rafiki za upimaji wa VVU ulivyoweza kuifikia jamii ya rika zote na jinsi zote na hata kuwa huduma rafiki kwa jinsi za kiume yaani wanaume, tunashauri serikali iendelee kutumia hiyo brand kwani tunaamini neno Angaza ni rafiki na linaondoa hofu na linaleta ujasiri hata kwa wanaokuwa na VVU," alisema Temu.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa, wanashukuru uthubutu wa wataalam wa wizara ya afya kuweza kuongeza wapimaji wa VVU kutoka kwa wataalam wa maabara hadi wahudumu wa afya walio wa maabara.

Alimalizia kwa kusema, wao Amref na wadau  wakiwemo SRs, wataendelea kufanya kazi kwa karibu na kufuata miongozo ya Global Fund, Sera na mitakati ya kitaifa, maelekezo ya vikao mbalimbali vya TNCM na hata kusimamia matumizi ya fedha za ufadhili huo na kutumia vyombo vilivyopo katika kutafuta ushauri ikiwemo wizara ya afya na vitengo vyake ambavyo ni Sekretariet ya TNCM,lfa PR-1 (Wizara ya Fedha) na Programme za NACP na NTLP pamoja na GF Office ya Wizara ya Afya.

Naye Dr. Ndugulile akizungumza katika uzinduzi huo, aliishukuru Amref na wadau wengine waliopewa jukumu la kupambana na maradhi ya kifua kikuu pamoja na Ukimwi ambao ni THPS, MDH, BMF na TAYOA.

Naibu waziri huyo aliwataka wote kuwa wabunifu na wenye mikakati ili kufikia malengo ya  kupambana na maradhi hayo kama walivyoyaanisha kwenye mchanganuo wa bajeti waliyoomba.

Alisema milango ipo wazi kwa wao kufika ofisini kwao kwa lengo la kuhitaji ushauri wowote watakaouhitaji.

Wednesday, May 23, 2018

CRDB, Jeshi la Magereza kuboresha uhusiano wa kibiashara

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei (kushoto) akizungumza na baadhi ya maafisa waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini, juu ya kuangalia njia bora za kudumisha uhusiano baina ya Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza nchini, katika Makao Makuu wa Magereza, jijini Dar es salaam, Mei 23, 2018. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa. 

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa akizungumza katika kikao na uongozi wa Benki ya CRDB, uliomtembelea ofinisi kwake, Makao Makuu ya Magereza jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei. 



Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei (kushoto) akimkabidhi zawadi maalum, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa, wakati alipomtembelea ofisini kwake, Makao Makuu wa Magereza, jijini Dar es salaam, Mei 23, 2018. Mkutano huo ulikuwa na lengo kudumisha uhusiano wa kibiashara baina ya Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza nchini. 


Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Dokta Juma Malewa alimshukuru Dokta Kimei kwa kutembelea Jeshi hilo na kuipongeza Benki ya CRDB kwa maboresho hayo katika huduma zake, huku akiisifu zaidi huduma ya Salary Advance ambayo alisema kwa kiasi kikubwa imesaidia kuboresha maisha ya askari. Dokta Malewa alisema katika maboresho hayo yanayoendelea Jeshi la Magereza lingependa kutumia mfumo wa kibenki katika kukusanya mapato yake katika miradi na huduma mbalimbali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato.

“Nikuombe Dokta Kimei na uongozi mzima wa Benki ya CRDB kuona uwezekano wa kuweka huduma za kibenki kama ATM na Matawi kwenye maeneo ya Magereza yenye uhitaji mkubwa wa huduma hiyo”, aliongezea Dokta Malewa. Dokta Malewa pia aliiomba Benki ya CRDB kushiriki katika miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa na Jeshi hilo ikiwamo ujenzi wa hospitali ya Jeshi la Magereza Ukonga, miradi ya Kilimo cha kisasa na chenye tija, mradi wa kokoto Msalato pamoja na uwekezaji katika miradi ya viwanda vidogo vidogo.
Baadhi ya Maafisa waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini, wakiongozwa na Naibu Kamishna wa Jeshi hilo, Kamishna Festo Sanga (wa kwanza kulia) wakati wa kikao maalum na uongozi wa Benki ya CRDB, uliotembelea Makao Makuu ya Magereza, jijini Dar es salaam leo.
“Ningependa kuona pia Benki ya CRDB kuwa mteja wa bidhaa na huduma zinazotolewa na Jeshi la Magereza mfano Benki kutumia samani za ofisi na Magereza kupewa Kandarasi za ujenzi wa miradi ya Benki inayodhaminiwa au kumilikiwa na Benki”, aliongezea Dokta Malewa akionyesha fursa ya kibiashara iliyopo baina ya Benki na Jeshi la Magereza.

Dokta Kimei alimhakikishia Mkuu wa Jeshi la Magereza kuwa Benki ya CRDB ipo tayari kushirikiana na Jeshi hilo katika miradi mbalimbali ambayo wamepanga kuitekeleza, huku akihaahidi kutuma timu ya wataalam kutoka Benki ya CRDB kufanya upembuzi yakinifu juu ya kuweka ATM na kufungua vito vya kutolea huduma katika maeneo ya Jeshi la Magereza ilikufikisha huduma kwa akari kwa urahisi.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akieleza jambo kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Juma Malewa (hayupo pichani) katika kikao kilichofanyika Makao Makuu ya Magereza, jijini Dar es salaam leo.

“Matarajio yangu ni kuona uhusiano baina yetu ukikua zaidi, naihidi kuwa kupitia Wakurugenzi na Mameneja wetu wa matawi tutaweka utaratibu wa kutembelea ofisi za Magereza nchi nzima ili kuhakikisha haya tuliyokubaliana hapa yanatekelezwa”, alisema Dokta Kimei.

Mkutano huo ulimalizika kwa Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza kutengeneza kikosi kazi cha kufuatilia utekelezaji wa maazimio ambapo Kamishna Gaston Sanga Mkurugenzi wa Utawala, fedha na Rasimali watu wa Jeshi la Magereza alichaguliwa kuwa Mwenyekiti akisaidiwa na Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na wakati wa Benki ya CRDB Bi. Jesica Nyachiro. Dokta Kimei pia alimuomba Mkurugenzi wa Masoko wa Benki ya CRDB Bi. Tully Mwambapa kuona namna ambavyo Benki ya CRDB itaweza kuunganisha shughuli zake za misaada kwa jamii na Jeshi la Magereza.


Katika mkutano huo Benki ya CRDB iliahidi kutoa msaada wa kompyuta na vitendea kazi vingine kwa Jeshi la Magereza ili kuongeza ufanisi wa Jeshi hilo. Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi April 2018, Benki ilikuwa pia imeshafungua zaidi ya Akaunti elfu tatu (3,000) za mishahara kwa askari wa Jeshi la Magereza.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei akizungumza.
Baadhi ya Maafisa wa Benki ya CRDB, wakiwa kwenye kikao hicho.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei (kushoto) akimkabidhi zawadi maalum, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa, wakati alipomtembelea ofisini kwake, Makao Makuu wa Magereza, jijini Dar es salaam, Mei 23, 2018. Mkutano huo ulikuwa na lengo kudumisha uhusiano wa kibiashara baina ya Benki ya CRDB na Jeshi la Magereza nchini.
Picha ya pamoja.

DAWA ZAVUSHWA KUPITIA MTO WENYE MAMBA MKOANI RUVUMA

 Wakazi wa vijiji vilivyopo kandokando ya mto Ruvuma wilayani Nyasa mkoani Ruvuma na wafanyakazi wa Bobari ya Dawa (MSD), wakisaidia kushusha maboksi yenye dawa na kuyaingiza kwenye mtumbwi baada ya kupelekewa na MSD Kanda ya Iringa leo na baadae kuyapeleka katika Zahanati ya Kijiji cha Mitomoni.
 Maboksi ya dawa yakiingizwa kwenye mtumbwi.
 Wakazi wa Kijiji cha Mitomoni wakisubiri mtumbwi ili kuwavusha upande wa pili wa mto Ruvuma.
 Dawa zikipelekwa Zahanati ya Mitomoni
 Maboksi ya dawa kutoka MSD yakishushwa
 Wananchi wakishusha maboksi hayo kutoka katika mtumbwi.
 Mkazi wa Kijiji cha Mitomoni Khadija Salum, akizungumzia upatikanaji wa dawa kutoka MSD.
 Mkazi wa kijiji hicho, Mbwana Koloma, akizungumzia changamoto ya miundombinu ya barabara na jinsi wanavyopokea dawa kutoka MSD.
 Mwenyekiti wa kamati ya Afya wa Kijiji cha Mitomoni Omar Hassan akizungumza wakati wa kupokea dawa hizo.
Mmoja wa viongozi wa Kijiji cha Nakawale, Ima Komba akisaini fomu maalumu ya kupokelea dawa kutoka MSD.

Na Dotto Mwaibale, Ruvuma

WANANCHI wanaoishi katika Vijiji vya Mkenda na Mitomoni vilivyopo kandokando ya mto Ruvuma wilayani Nyasa mkoani Ruvuma wamesema changamoto kubwa waliyonayo ni 
mazingira magumu ya miundo mbinu ambayo inasababisha ugumu wa ufikishaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kutoka  Bohari ya Dawa (MSD).

Wakazi hao wamesema kuwa, mazingira ya kufikisha dawa kwenye vijiji hivyo hutegemea zaidi usafiri wa kuvuka mto Ruvuma ambapo hulazimika kutumia boti,ambapo hata hivyo maisha yao yanakuwa na mashaka ndani ya mtumbwi hiyo ambayo iko wazi kutokana na mto huo kuwa na mamba wengi.

"Changamoto yetu kubwa ni usafishaji wa dawa kuja hapa kijijini kutokana na kutegemea zaidi mto huu ambao una mamba wengi, hata mwaka huu mwanzoni mtumbwi huu mnaouona ulipinduka na watu  wakiwapo wauza mitumba waliuawa na mamba; lakini tunashukuru  Bohari ya Dawa (MSD) kwani wao wanaweza kutuletea dawa  kwa wakati" alisema Mwenyekiti wa kamati ya Afya wa kijiji cha Mitomoni Omar Hassan.

Alisema ili kuondoa changamoto hiyo, wanaiomba serikali kuhakikisha inaboresha miundombinu ya barabara, ili dawa hizo zisafirishwe kwa njia ya barabara badala ya kutegemea mto huo. 

Alisema yeye na kamati yake wamekuwa wakipokea dawa mara nne kwa mwaka kutoka MSD na kuzihakiki kwa ajili ya matumizi.

"Pamoja na changamoto ya miundombinu lakini tumekuwa tukihakikisha dawa zinazoletwa na MSD zinafika kituoni na kutumika ipasavyo,"alisema.

Alisema kutoka Songea mjini hadi Kijiji cha Mitomoni, Songea vijijini, katika kituo hicho cha afya ni km 135 na MSD imekuwa ikihakikisha dawa hizo zinafika.

Alisema changamoto zinakuwa kubwa zaidi kipindi cha mvua kwa kuwa miundombinu ya barabara hadi kufika kivukoni ni tatizo na kuna wakati dawa zinafika usiku na zinatakiwa kuvushwa usiku huo huo.

Hassan alisema changamoto hiyo ya mamba katika mto huo anaijua vizuri kwani mtoto wake Sanifu Omar (27), alipoteza maisha kwa kuliwa na mamba wakati alipokuwa akisafirisha abiria kwa kutumia mtumbwi.

Mkazi wa Kijiji cha Mitomoni Khadija Salum alisema wamekuwa wakipata dawa zote muhimu katika kituoni hicho ikiwemo za mama mjamzito na mtoto bila ya ubaguzi na kwa wakati.

"Mimi nina watoto watano kuanzia ujauzito wa kwanza sijawahi kukosa dawa hapa pamoja na ugumu wa miundombinu lakini dawa zinafika hivyo serikali ione haja ya kuboresha barabara zetu," alisema.

Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mitomoni, Ivo Hekela, alisema kijiji hicho kinahudumia agonjwa 12,000 kutoka vijiji vitano ambavyo ni Mitomoni, Mipotopoto,Konganywita,Mkenda,Uhuru na Mozambique. 

Meneja wa MSD Kanda ya Iringa, John Sipendi, alisema wamekuwa katika changamoto ya kufikia vituo hivyo vya pembezoni ikiwa ni pamoja na kutumia muda mrefu kufikisha dawa na wakati wa mvua kukwama kwa magari njiani na gharama za usafirishaji kuogezeka.

Madereva wa MSD Kanda ya Iringa wamesema wamekuwa wakishindwa kushusha dawa wakati wa mvua za masika kutokana na mto huo kujaa maji hivyo hulazimika kulala kijijini hapo kwa siku mbili hadi tatu.

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...