Wednesday, April 27, 2011

Irani yatoa USD mil 1.2 kusaidia Kilimo Kwanza

Naibu Waziri Nyarandu

Na Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Irani imepanga kutoa dola za kimarekani milioni 1.2 (dola milioni 1.2) kuisaidia Tanzania katika utekelezaji wa vitendo kampeni za Kilimo Kwanza.
Taarifa imetolewa leo jijini Dar es Salaam wakati Balozi Msaidizi wa Iran nchini Tanzania Bahman Ahmadi alipotembelea Wizara ya Viwanda na Biashara na kuzungumza na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Lazaro Nyalandu.
Katika mazungumzo hayo yaliyojikita zaidi kuimarisha uhusiano mzuri kibiashara baina ya nchi hizo mbili, Nyalandu kwa niaba ya Serikali ya Tanzania ameishukuru Iran kwa msaada huo na kuahidi kuwa utatumika kama ulivyokusudiwa.

Hata hivyo Naibu Waziri huyo amewakaribisha wawekezaji kutoka Iran kuja nchini na kushirikiana na wazalendo katika kutumia vema fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya kilimo.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...