Saturday, January 20, 2018

Watoto Mwanza wataja 'kichocheo' cha mimba za utotoni

Watoto wakiwa katika mafunzo ya siku tatu kwa wafanyakazi wa nyumbani Jijini Mwanza, kuhusu Elimu ya Afya ya uzazi yaliyoandaliwa na Shirika la Kutetea Haki za Watoto Wafanyakazi wa Nyumbani nchini WOTESAWA.


George Binagi-GB Pazzo

WATOTO wafanyakazi wa nyumbani Jijini Mwanza wameeleza kwamba suala la ukosefu wa elimu ya afya ya uzazi ni chanzo kikuu cha tatizo la mimba za utotoni na hivyo kuomba elimu hiyo izidi kutolewa katika makundi mbalimbali ya watoto ili kupambana na tatizo hilo.

Watoto hao waliyasema hayo jana kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wafanyakazi wa nyumbani Jijini Mwanza, kuhusu Elimu ya Afya ya uzazi yaliyoandaliwa na Shirika la Kutetea Haki za Watoto Wafanyakazi wa Nyumbani nchini WOTESAWA.

“Ukosefu wa elimu ya uzazi, umaskini, tamaa pamoja na makundi maovu yenye ushawishi ni miongoni mwa sababu zinazosababisha mimba za utotoni hivyo mafunzo haya yatatusaidia kuepukana na tatizo hilo”. Alisema Christina William ambaye ni mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo.

Akiwasilisha mada kuhusu mimba za utotoni, Veronica Rodrick ambaye ni Afisa Miradi shirika la WOTESAWA, alisema ni wakati mwafanya wazazi na walezi nchini kuvunja ukimya na kuzungumza na watoto wao kuhusu afya ya uzazi ili kuwanusuru na mimba za utotoni pamoja na magonjwa ya zinaa.

“Tumeamua kuvunja ukimya kwa sababu inaonekana hata huko nyumbani wazazi wanaogoka kukaa na watoto wao kuzungumza juu ya masuala ya afya ya uzazi ikiwemo mimba, virusi vya ukimwi na kinga”. Alisisitiza huku akiwahimiza kujiepusha na mapenzi katika umri mdogo, na hata ikitokea mtu ameshindwa kujizuia basi wazingatie matumizi ya kondom.

Katika mada hiyo, kulikuwa na mjadala mpana juu ya matumizi sahihi ya kondom ambapo walihoji ikiwa ni kweli kondomu inazuia mimba pekee ama inazuia pia na magonjwa ya kuambukiza ikiwemo virusi vya ukimwi, hatua iliyoashiria kwamba watoto wengi katika ya miaka 14 hadi 18 bado hawana elimu ya kutosha kuhusu elimu hiyo.

Baadhi ya watoto walikuwa wakiamini kwamba kondom inazuia mimba pekee na haiwezi kuzuia virusi vya ukimwi huku wengine wakiamini kondom zina vitundu vidogo vidogo vinavyoweza kupitisha virusi vya magonjwa ya kuambukiza, jambo ambalo si sahihi kwani matumizi sahihi ya kondom huzuia mimba na maambukizo ya magonjwa ya kujamiana.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...