Tuesday, January 2, 2018

Vijana wa Chama Cha Mapinduzi waridhishwa na utekelezwaji na miradi ya afya

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akipokewa na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi  Nzega- mkoa wa  Tabora  akiwa anaelekea Mwanza kwa ajili ya mapokezi yake baada ya kuchaguliwa na mkutano mkuu wa 9 wa UVCCM kuwa mwenyekiti mpya wa UVCCM 2017-2022. 

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Kheri Denice James akizungumza na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake wilayani Nzega Mkoa wa Tabora (hawapo pichani).

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akitunza fedha katika kikundi cha ngoma ya Asili alipowasili Wilaya ya Nzega Vijijini kuzungumza na Viongozi mbali mbali wa chama.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akipata maelezo toka kwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Ndugu Amos Kanuda na Mkuu wa wilaya ya Nzega Ndugu Godfrey William Ngupula,alipotembelea kituo cha afya cha Zogolo kilichopo Halmashauri ya mji wa Nzega kinachotegemewa zaidi kuhudumia wananchi wa mji wa Nzega yenye watu wasiopungua laki mmoja. Ujenzi unaolenga kuboresha utoaji wa huduma katika kituo hiki ulikadiriwa kugharimu shillingi milioni 500 ukiwa ni ufadhili wa mfuko wa World Bank.


Na Mwandishi wetu, Tabora 

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) umesema umeridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya afya inayotokana na ahadi katika ilani ya uchaguzi katika halmshauri za wilaya mji wa Nzega na Nzega vijijini mkoani Tabora.

Pia Umoja huo umeeleza kikubwa kasi hiyo inatokana na kuwepo kwa mashirikiano makubwa kati ya viongozi wa chama, Halmashauri za wilaya na serikali kuu.

Matamshi hayo yametamkwa jana na Mwenyekiti wa Taifa wa UVCCM Kheri Denise james mara baada ya kumaliza kutembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya cha Kazogolo katika Halmashauri ya Mji wa Nzege.

Kheri alisema kitendo cha serikali ya awamu ya tano kupeleka jumla ya shilingi milioni mia tano toka serikali kuu oktoba mwaka huu  kwa ajali ya ujenzi wa kituo hicho ni kielelezo kuwa serikali inajali maisha ya wetu wake .

"UVCCM tumeridhishwa na ujenzi wa miradi ya afya katika Halmashauri ya Mji wa Nzega na Halmashauri ya Nzega vijijini. Ilani ya uchaguzi ya chama imetekelezwa kwa vitendo. Hii ndiyo tafsiri halisi ya hapa kazi," Alisems Kheir .

Aidha alisema kazi ya kuwatumikia wananchi haina mjadala badala yake inamhitaji kila kiongozi dhamana kuwa nafasi yake kuwajibika na kuwatumikia wananchi.

"Kuimarika kwa huduma za jamii na watu kupata huduma bora ndiyo malengo ya kisera yanayotakiwa kufanikishwa. Tuna wajibu kila mmoja kwa nafasi yake kumsaidia Rais na serikali yale." Alisisitiza.

Kheri akiwa mkoani Tabora ametembelea mradi mkubwa wa usambazaji maji toka ziwa Victoria mkoani mwanza kupitia shinyanga hadi Tabora, kuona maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya kazogolo na kuzumgumza na wananchi katika halmashsuri ya mji wa nzega na nzega vijiijini. 

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...