Tuesday, March 29, 2011

Obama aeleza sababu za kumpiga Gadhafi


Rais wa Marekani, Barrack Obama

RAIS Barrack Obama wa Marekani, ameeleza sababu za kuingilia mgogoro uliokuwa ukiendelea nchini Libya, kati ya Rais wa nchi hiyo, Moammar Gadhafi na waasi waliokuwa wakimpinga na maandamano yaliokuwa yakifanywa na makundi ya wananchi nchini humo.

Miongoni mwa sababu ya msingi ambazo Obama amewaeleza waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani, ni kwamba waliamua kufanya hivyo ili kunusuru maisha ya wana-Libya waliokuwa wakiuawa na majeshi ya Serikali yaliokuwa yakiwazuia waandamanaji waliokuwa wakimpinga Gadhafi.

Obama alisema nchi yake isingelipenda kuona wananchi wakiuawa na kunyanyasika ilhali hawana hatia na ndio maana yeye (USA) na washirika wake walifanya uamuzi wa kuivamia Libya kwa lengo la kumuondoa Gadhafi madarakani.

"Tunamalizia kufanya mashambulizi ya mwisho kwenye mji ambao ulikuwa makazi na ngome ya Gadhafi lakini baada ya hapo tutakabidhi madaraka ya kuiongoza nchi ya Libya kwa Jeshi la NATO, ili waweke utaratibu wa nchi kurudi wakati wake," alisema Obama akionekana kujiamini.

1 comment:

  1. WIZI MTUPU!!!!!!!!!!! SI ASEME TU NI HAYO MAFUTA MBONA ANADIVET

    ReplyDelete

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...