Tuesday, March 22, 2011

Jambo Leo wawafanya vibaya TBC1 kombe la NSSF



Baadhi ya wachezaji wa Jambo Leo katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo wao na TBC1.


TIMU ya Soka ya Gazeti la Jambo Leo, linalomilikiwa na kampuni ya Jambo Concepts Ltd, imeshindilia timu ya Soka ya Shirika la Habari Tanzania (TBC 1) mabao 3 kwa moja.

Wakicheza mpira ulioonekana wa hali ya juu kiasi cha kuwapa tabu muda wote, TBC1 Jambo Leo ndio walioanza kuanza kufungua mvua ya magoli baada ya muda mfupi tangu kuanza kwa pambano hilo.

Goli la kwanza la Jambo Leo, liliwachanganya zaidi washambuliaji wa TBC1 na kujitahidi kusawazisha muda mfupi baadaye kabla ya mapumziko. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi hasa kwa wachezaji wa Jambo Leo ambao walionekana kuwaelemea zaidi TBC1 na kuandika mabao mawili mengine ya harakaharaka.

Hadi mwisho wa mchezo huo Jambo Leo 3 na TBC1 waliambulia goli moja.


Benchi la ufundi la Jambo Leo pamoja na wachezaji wa akiba. Watatu kulia waliokaa ni Mkurugenzi Msaidizi wa Jambo Concepts Ltd, Benny Kissaka akifuatilia vijana wake.




Kikosi kizima cha timu ya Jambo Leo kikiwa na kocha wake (wa kwanza kushoto waliosimama) na kiongozi wa benchi la ufundi (wa pili waliosimama) kabla ya kuanza kwa pambano kati ya TBC1 na timu hiyo.

Waamuzi wa mchezo huo wakiwa katika picha ya pamoja, kabla ya kuanza kwa pambano.




Kikosi cha TBC1 kilichoshindiliwa 3-1 katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo huo. Picha na Mdau Mkuu wa Harusi na Matukio.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...