Thursday, March 17, 2011

Picha mbalimbali za ziara ya NSSF Bukoba na Mwanza kukagua miradi yao



Meneja wa Kiwanda cha Sukari Kagera, Nestory Ruchungura (wa kwanza kulia aliye nyoosha mkono mbele) akitoa maelekezo kwa baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) walipotembelea kiwanda hicho juzi mjini Kagera. 


Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Sukari cha Kagera, Ashwin Rana akitoa maelezo mafupi ya kiwanda hicho kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya NSSF walipotembelea kiwanda hicho hivi karibuni.








Meneja wa Kiwanda cha Sukari Kagera, Nestory Ruchungura (wa kwanza kulia aliye nyoosha mkono mbele) akitoa maelekezo kwa baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) walipotembelea kiwanda hicho juzi mjini Kagera. 


Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya NSSF (waliosimama msitari wa mbele) wakipiga picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya viongozi wa juu wa Kiwanda cha Sukari cha Kagera (waliosimama nyuma). Wapili kushoto mbele ni Meneja Mkuu Msaidizi wa Kiwanda, Buddana Rau. Nyuma ni moja ya matrekta ya kisasa yalionunuliwa na kiwanda hicho baada ya mkopo wa NSSF kwa kiwanda hicho, matrekta hayo yanauwezo wa kufanya kazi yenyewe kwa msaada mdogo wa dereva.


Miongoni mwa matrekta ya kisasa yaliyonunuliwa na kiwanda hicho baada ya kupata ufadhili wa mkopo wa takriban bilioni 12 kutoka NSSF



Kutoka kushoto ni Mwenekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Abubakar Rajab (mwenye koti), Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Sukari cha Kagera, Ashwin Rana, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Ramadhan Dau na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi NSSF, Mudhihir Mudhihir wakiwaongoza wajumbe wengine wa NSSF kutembelea kiwanda hicho. NSSF imetoa ufadhili wa mkopo wa sh. bilioni 12 kwa kiwanda hicho.








No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...