Monday, February 21, 2011

Mabomu yalivyoitetemesha Dar es Salaam

Februari 16/17 huenda ikabaki historia ya pekee dhidi ya tukio la milipuko ya mabomu yaliyotokea katika Kikosi namba 511 cha Jeshi la Wananchi (JWTZ) kilichopo eneo la Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.
Zifuatazo ni baadhi ya picha zikionesha namna wakazi wa maeneo ya Jiji la Dar es Salaam, hasa Gongo la Mboto walivyoathiriwa na mabomu siku hiyo na siku iliyofuatia.




Baadhi ya wananchi akiyakimbia maeneo ya milipuko siku ya kuamkia milipuko ya mabomu, wakihofia maeneo hayo si salama tena. Hata hivyo tetesi za uwongo ndiyo kilichoendelea kuyakimbia maeneo hayo, baadhi ya vibaka waliwaongopea wakazi kuwa yangelipuka mengine baadaye.



Watu walilazimika kubeba kile walichoweza na kutembea kwa muda mrefu. Hata hivyo ungelibahatika kumuuliza mmoja wao kuwa alikuwa akielekea wapi hawa kuwa na jibu zaidi ya kusema "hatujui"



Uwanja wa Uhuru ghafla ulibadilika na kuwa kambi ya kuwahifadhi 'wakimbizi' wa muda wa makazi yao, hawa waliopangwa na kukaa chini ni watoto zaidi ya mia 400 ambao walipotezana na wazazi wao. Uwanja huo ulipokea zaidi ya watu 4000 kwa siku moja.



Viongozi wa Kuu wa nchi kesho yake ya siku ya milipuko yaani Februari 17 walilazimika kuyatembelea eneo la Jeshi lililotokewa na milipuko hiyo, pichani ni Rais Jakaya Kikwete (aliyevaa miwani) akiwa na Mkuu wa JWTZ, Davis Mwamunyange alipokitembelea kikosi 511 ilipotokea milipuko.



Mabaki ya mabomu yalizagaa mitaani kwenye makazi ya watu, magari ya jeshi na polisi walilazimika kupita na kuyakusanya moja baada ya lingine. Gari likiwa limepakia shehena ya baadhi ya mabomu. Picha zote na mdau wa Harusi na Matukio. 

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...