Friday, February 25, 2011

Bei ya Sukari kushuka


Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami (Kushoto) na Naibu wake, Lazaro Nyalandu(Kulia) katika mkutano na waandishi wa Habari.


SERIKALI imefuta ushuru wa forodha kwa sukari kiasi cha tani 37,500 itakayoagizwa toka nje ya nchi za Afrika ya Mashariki, jambo ambalo linaweza kusababisha bei ya sukari kushuka nchini.
Agizo hilo limetolewa jana na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami katika taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa baada ya kikao na wadau wa sukari nchini.

Waziri amesema kiasi cha tani 12,500 zitaagizwa toka nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika ya Mashariki hakihitaji kufutiwa kodi kwa kuwa hakuna tozo zozote kwa bidhaa hiyo.

Kutokana na mahitaji hayo kiasi cha tani 50,000 za sukari toka nje ya nchi, na kwa kuwa bei ya sukari katika soko la dunia imepanda kwa sasa, Serikali imeiagiza Mamlaka ya Bandari iweke utaratibu mahsusi wa kutoa kipaumbele kwa meli zitakazoleta sukari hiyo ili zipakuliwe haraka na kuifanya sukari imfikie mlaji mara moja.

Aidha, Mamlaka ya Mapato (TRA) wanaagizwa wachukue hatua za haraka kukamilisha taratibu za kutotoza ushuru wa forodha kwa sukari hiyo.

Serikali itaendelea kushirikiana na wadau katika sekta ndogo ya sukari ili kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa hii kwa bei nafuu. Ni imani ya Serikali kuwa kwa kuwa utekelezaji wa hatua hizi unaanza mara moja, mambo mawili yatatokea. La kwanza, sukari itamfikia kila Mtanzania popote alipo.

La pili, bei ya sukari itashuka; na kwa vyovyote vile, pamoja na bei kupanda katika soko la Dunia, Serikali inategemea kuwa bei ya sukari itakuwa chini ya sh. 1,700 kwa kilo, hata katika maeneo ya pembezoni kabisa, Aidha, Serikali imeweka utaratibu wa kukutana na wazalishaji na wasambazaji wa sukari mara kwa
mara ili kuongeza uzalishaji wa sukari nchini chini ya mpango wa Kilimo Kwanza na hivyo kuondoa tatizo la upungufu wa sukari nchini.

Mwisho

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...