Thursday, February 3, 2011

JK ana kwa ana na Mbowe

Jk akisalimiana na Mbowe

WANASEMA mpinzani wa kisiasa si ugomvi japokuwa kwa upande wa wanachama huwa ni tofauti kwa upinzani wa vyama. Viongozi wa juu wao wanapokutana husahau yote ya nyuma na kufanya shughuli zao kama kawaida tena kwa fura.

Ndivyo ilivyoonekana Februari 2 jijini Dar es Salaam baada ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM kukutana na mpinzani wake mkumbwa kisiasa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya Sheria nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo Rais Kikwete aliyekuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Mahakama Kuu.

Aliwataka watumishi wa mahakama kutambua kuwa mahakama zimewekwa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi, hivyo wanatakiwa kutenda yale yanayostahili ikiwa ni pamoja na kutenda haki.

“Kuna fununu zimekuwa zikienea kuwa katika tasnia hii kuna vitendo vya rushwa vilivyokithiri, lakini iwapo mtafabya kazi kwa uadilifu na kwa kujali maslahi ya wananchi basi malalamiko hayo yataisha kwani haki itakuwa imetendeka,” alisema Rais Kikwete.

Alisema uamuzi wa mahakama ni wa mwisho hauwezi kutenguliwa na yeyote nchini. “Mara kadhaa nimekuwa nikipokea malalamiko na maombi ya msaaada kutoka kwa waliohukumiwa kesi mbalimbali, wengi wamekuwa wakidhani kuwa mimi nina uwezo wa kutengua kilichotolewa na mahakama jambo ambalo si kweli. Na mara nikiwajibu kuwa siwezi kufanya hivyo, huwa wananieleza kuwa sio kweli na kwamba wanaamini kuwa nimeshindwa kufanya kazi,” alisema Rais Kikwete


Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na jopo la majaji, Akiwemo Spika wa Bunge Anna Makinda na Waziri wa Sheria na Katiba, Selina Kombani.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...