Tuesday, February 27, 2018

Benki ya NMB yafungua tawi jipya Ruaha, Iringa

Mkuu wa mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi 
la NMB Ruaha Mkoani Iringa. Tawi hili litakua ni tawi linafikisha idadi ya matawi 214 ya NMB nchi 
Nzima. Kushoto ni Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini, Badru Idd na Mkuu wa Kitengo cha wateja wadogo na wakati, Abdulmajid Nsekela (kulia) wakishuhudia tukio hili lililofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Iringa

Mkuu wa mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi 
la NMB Ruaha Mkoani Iringa. Tawi hili litakua ni tawi linafikisha idadi ya matawi 214 ya NMB nchi 
Nzima. Kushoto ni Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini, Badru Idd na Mkuu wa Kitengo cha wateja wadogo na wakati, Abdulmajid Nsekela (kulia) wakishuhudia tukio hili lililofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Iringa

Mkuu wa mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi 
la NMB Ruaha Mkoani Iringa. Tawi hili litakua ni tawi linafikisha idadi ya matawi 214 ya NMB nchi 
Nzima. Kushoto ni Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini, Badru Idd na Mkuu wa Kitengo cha wateja wadogo na wakati, Abdulmajid Nsekela (kulia) wakishuhudia tukio hili lililofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Iringa


BENKI ya NMB Tanzania imezindua tawi jipya Ruaha ambalo limeanzishwa kwa lengo la kusogeza
huduma za kifedha karibu zaidi na wananchi wa mkoa wa Iringa.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tawi hilo, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa
Kati wa NMB Bw. Abdulmajid Nsekela alisema,” Benki ya NMB imeendelea kuwa benki yenye
mtandao mpana zaidi wa matawi na ATM; tawi hili likiwa ni la 214 na ATM zaidi ya 800 nchi
nzima huku ikiwa na mawakala wanaotoa huduma za NMB zaidi ya 4000 nchi nzima huku ikijivunia wateja wake zaidi ya milioni 3.

“Mafanikio haya yasingeelezwa leo kama si kuaminiwa na wateja wetu ambao miongoni mwao ni
wana Ruaha na Iringa kwa ujumla kuwa benki wanayoipendelea zaidi na hivyo kuwa ni benki
yenye mafanikio makubwa zaidi nchini.”

Pamoja na ufunguzi wa tawi hilo, pia benki ya NMB ilitoa msaada wa milioni 5 ambazo zitaelekezwa katika sekta ya afya na elimu, ambapo Nsekela aliitaka serikali kusema ni maeneo gani ingependa pesa hiyo itumika.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...