Wednesday, November 8, 2017

COSTECH yawapa wanafunzi Sikonge mbegu ya viazi lishe

 Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa (kulia), akimkabidhi mbegu ya mahindi aina ya Wema, Mkuu wa Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora, Peres Boniface Magiri wakati wa uzinduzi na kukabidhi mbegu bora za Mahindi ya Wema 2109, mihogo na viazi lishe kwa ajili ya mashamba darasa katika vijiji vya Isunda, Kisanga, Udongo na Kanyamsenga wilayani humo jana.
 Wanakikundi cha Aliselema wakishusha mbegu ya mihogo tayari uzinduzi wa shamba darasa.
 Ofisa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Said Babu akizungumza kabla ya kuanza uzinduzi huo katika Kijiji cha Isunda kilichopo Kata ya Nkolye.
 Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Pares Magiri akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Isunda.
 Wanakikundi cha Aliselema wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Mtafiti wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku kilichopo mkoani Kagera Jojianas Kibura akielekeza namna ya kupanda mihogo.


  Mtafiti wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku kilichopo mkoani Kagera Jojianas Kibura akimuelekeza namna ya kupanda mbegu ya mihogo mkuu wa wilaya hiyo.
 Mwenyekiti wa Kikundi cha Aliselema, Amir Hassan akipanda mbegu ya mihogo.
 Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa akipanda mbegu ya mihogo katika shamba darasa.
 Mwenyekiti wa Kikundi cha Aliselema, Amir Hassan akizungumza na waandishi wa habari kuhusu changamoto waliyokuwa nayo ya kupata mazao kiduchu kwa kutumia mbegu zisiso bora.

 Wakulima wakisubiri kuelekezwa namna ya upandaji wa mbegu hizo za mihogo.
 Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Pares Magiri akizungumza na wakulima wa Kijiji cha Kisanga kabla ya uzinduzi wa shamba darasa la viazilishe.
 Mtafiti wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku kilichopo mkoani Kagera Jojianas Kibura akimuelekeza namna ya kupanda mbegu ya viazilishe katika kijiji cha Kisanga.
 Wanawake wa Kijiji cha Kisanga wakiwa kwenye uzinduzi huo wa shamba darasa la mbegu ya viazilishe.
 Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti cha Ukiriguru mkoani Mwanza, Mariana akielekeza namna ya upandaji wa viazilishe.
 Mkuu wa Wilaya, Peres Magiri akipanda mbegu ya viazilishe wakati wa uzinduzi wa shamba hilo.
 Mwalimu wa Baraka Kita wa Shule ya Msingi Sogea B, akipanda mbegu hiyo ya viazilishe.
 Mkulima, Mariam Said akipanda mbegu ya viazilishe 
Mwalimu George Adamu Mwalwizi, akizungumzia mbegu mpya ya viazi lishe walioletewa kuwa itakuwa ni mkombozi kwao na wanafunzi.

Na Dotto Mwaibale, Sikonge Tabora

WANAFUNZI wilayani Sikonge mkoani Tabora wataanza kunufaika na viazi lishe baada ya kupokea mbegu bora ya viazi hivyo, mihogo na mahindi ya Wema kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB)

Hayo yameelezwa katika Kijiji cha Kisanga na Mkuu wa Wilaya hiyo, Peres Boniface Magiri wakati akizungumza na wakulima kwenye uzinduzi na kukabidhi mbegu bora za Mahindi ya Wema 2109, mihogo na viazilishe kwa ajili ya mashamba darasa katika vijiji vya Isunda, Kisanga, Udongo na Kanyamsenga.

Magiri alisema baada ya kuotesha mbegu hiyo ya viazilishe kwa wingi kitakachofuata ni kuanzisha utaratibu wa wanafunzi katika shule mbalimbali za wilaya hiyo kupata chakula cha mchana badala ya kwenda nyumbani.

Alisema wilaya hiyo kupelekewa mbegu hizo kwao ni fursa kubwa na kwa kushirikiana na wakulima na maofisa ugani atahakikisha mashamba darasa hayo yanatunzwa na kutoa mrejesho.

Aliongeza kuwa shule mbalimbali zitaanzisha mashamba ya viazilishe hivyo ili kumaliza tatizo la kukosa chakula kama sio kulipunguza.

"Tunahitaji matokeo chanya ya mashamba darasa hayo yawasaidie wakulima wengine katika wilaya hiyo na kuwa atahakikisha anatembelea mara kwa mara yalipo mashamba hayo" alisema Magiri.

Mtafiti wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku kilichopo mkoani Kagera Jojianas Kibura aliwaambia wakulima kuwa hekta moja ya muhogo kwa kutumia mbegu hiyo bora inaweza kutoa tani 25 hadi 32 wakati viazi itatoa tani 7 hadi 9 kwa Hekta moja.

Alisema kuwa endapo watafuata kanuni bora za kilimo cha mazao hayo kwa kuzingatia nafasi kati ya mche na mche na mstari kwa mstari na matumizi ya mbolea wataweza kuongeza uzalishaji zaidi tofauti na sasa ambapo kwenye hekta moja ya muhogo wanapata tani nane hadi kumi wakati kwenye viazi wanapata tani moja hadi 3.

Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa, alisema mbegu hiyo ya mahindi imefanyiwa utafiti na inavumilia ukame wakati ile ya mihogo ikivumilia magonjwa kama batobato na michirizi kahawia huku zikitoa mavuno mengi.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...