Friday, October 30, 2015

Rais Mteule Dk Magufuli na Makamu Wake Wakabidhiwa Hati ya Uteuzi Dar

Baadhi ya wanaCCM na wananchi wengine walioshiriki hafla ya kukabidhiwa hati za uteuzi kwa Rais mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli pamoja na Makamu wake Mama Samia Suluhu Hassan leo  jijini Dar es Salaam.
Viongozi mbalimbali waandamizi wa taifa wakiwa katika hafla ya kukabidhiwa hati za uteuzi kwa Rais mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli pamoja na Makamu wake Mama Samia Suluhu Hassan leo  jijini Dar es Salaam.
Rais mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli (wa pili kulia) pamoja na Makamu wake Mama Samia Suluhu Hassan (nyuma yake) leo  jijini Dar es Salaam wakiwa katika hafla ya kukabidhiwa hati.
Meza kuu katika hafla hiyo Diamond Jubilee Dar es Salaam.
Viongozi mbalimbali wakishiriki kuimba wimbo wa taifa katika hafla hiyo.
Viongozi mbalimbali wakiwakilisha mataifa yao, mabalozi na waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wakiwa katika hafla hiyo.
Jaji mstaafu Damian Lubuva (kulia) akimkabidhi hati ya uteuzi Rais wa Tanzania anayesubiri kuapishwa, Dk. John Pombe Magufuli (kushoto) kwenye hafla maalum iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubelee Dar es Salaam leo.
Kushoto ni makamu wa Rais anayesubiri kuapishwa, Mama Samia Suluhu Hassan akionesha hati ya uteuzi wa nafasi hiyo mara baada ya kukabidhiwa na Jaji Damian Lubuva leo jijini Dar es Salaam.
Dk. Magufuli akimuonesha hati ya uteuzi Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete, wa kwanza kulia ni Makamu wake Mama Suluhu.
Viongozi mbalimbali wakiwakilisha mataifa yao, mabalozi na waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wakiwa katika hafla hiyo.
Wananchi na wanaCCM wakishangilia jambo katika hafla hiyo.
Dk. Magufuli akipunga mkono juu ya gari akitokea Ukumbi wa Diamond Jubilee kupokea kiapo cha uteuzi.
Dk Jakaya Kikwete akizungumza katika hafla hiyo.
Dk. Magufuli akizungumza ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam mara baada ya kupokewa.
Dk. Magufuli akizungumza ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam mara baada ya kupokewa.
Rais mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli akionesha hati ya uteuzi walizokabidhiwa na Tumea ya Taifa ya Uchaguzi kwa wanaCCM na wananchi waliofika kumlaki katika ofisi ndogo za CCM jijini Dar es Salaam leo

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...