Saturday, September 23, 2017

Prof Mbarawa alitaka Baraza la Ujenzi kuainisha gharama za miradi

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akihutubia wakati wa ufunguzi wa Semina ya siku moja ya wadau wa sekta ya ujenzi iliyohusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), jijini Dar es Salaam jana.


  Mwenyekiti wa Baraza hilo Mayunga Nkunya (wa tatu kushoto) akimpongeza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa baada ya kutoa hutuba yake.

 Mwenyekiti wa Baraza hilo Mayunga Nkunya, akitoa hutuba katika semina hiyo.

 Wadau wa sekta ya ujenzi.

 Taswira ya ukumbi wa semina.

Wadau wa sekta ya ujenzi wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Waziri Mbarawa.

Na Dotto Mwaibale

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameliagiza Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) kuhakikisha linaanisha gharama za Ujenzi wa miradi mbalimbali badala ya kutegemea makadilio ya Wakandarasi wanaopetekeleza miradi. 

Alisema hayo Jijini Dar es salaam jana wakati akifungua Semina ya Wadau wa Ujenzi iliyoandaliwa na Baraza la Taifa la Ujenzi ambapo amesema kutokan na utaratibu mbovu uliopo hivi sasa Watanzania wanatumia hata vifaa visivyokuwa na ubora wowote. 

"Sekta ya ujenzi ina mchango mkubwa katika kukuza pato la taifa na huwezesha utekelezaji wa miundombinu mbalimbali kuimarika na kuwa kichocheo  kikubwa kwa sekta nyingine za kiuchumi ikiwe kilimo,utalii nishati na viwanda" alisema Mbarawa. 

Mwenyekiti wa Baraza hilo Mayunga Nkunya amemhakikishia Waziri huyo kuwa changamoto zote zilizopo kwenye Sekta hiyo zitajadiliwa katika Semina hiyo na kupatiwa majibu ili kuepusha hasara na athari ambazo zinaweza kulikumba Taifa endapo hatua hazitachukuliwa. 

Alisema changamoto ambazo waziri amewapa amezitoa kwa baraza watazisimamia vizuri na kuhakikisha viwango vya ujenzi vinatekelezeka kwa lengo la kuimarisha  ubora wa majengo na miundombinu kwa ujumla. 

Aliongeza kuwa kutokana na kukosekana kwa Ushirikiano kutoka kwa wadau wa Ujenzi ndio sababu za changamoto hizo kujitokeza hivyo kupitia mkutano huo anaamini watafungua sura mpya ya maendeleo katika sekta hiyo na taifa kwa ujumla.


No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...