Thursday, April 14, 2016

NMB Yasaini Mkataba na MCFKutoa Mikopo kwa Hospitali Binafsi

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Ukopeshaji Vifaa vya Afya Hospitalini (MCF), Bi. Monique Dolfing- Vogelenzang (kushoto) kwa pamoja wakisaini mkataba wa makubaliano na kushirikiana kuzikopesha Hospitali na Vituo vya Afya Binafsi vifaa kwa ajili ya kuviwezesha kutoa huduma. Katika Makubaliano hayo NMB itatoa mikopo nafuu kwa Hospitali zinazohitaji baada ya kuratibiwa na MFC. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Ukopeshaji Vifaa vya Afya Hospitalini (MCF), Bi. Monique Dolfing- Vogelenzang (kushoto) wakibadilishana nakala za mikataba mara baada ya hafla ya kusaini mikataba hiyo kumalizika, Makao Makuu ya Benki ya NMB jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker (katikati) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari namna ambavyo Hospitali Binafsi ziotakavyonufaika na mikopo nafuu ambayo itatolewa kwa wahitaji mara baada ya kupata mafunzo na ushauri toka kwa mfuko wa MCF. Kulia ni Kaimu Ofisa Mkuu wa Wateja wadogo Benki ya NMB, Abdulmajid Nsekela na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa MCF, Bi. Dolfing- Vogelenzang. Mikopo inayotolewa itaanzia USD 15,000/- hadi USD 1,000,000/- kulingana na mahitaji ya kituo au hospitali yenyewe.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Ukopeshaji Vifaa vya Afya Hospitalini (MCF), Bi. Monique Dolfing- Vogelenzang (kushoto) wakibadilishana nakala za mikataba mara baada ya hafla ya kusaini mikataba hiyo kumalizika, Makao Makuu ya Benki ya NMB jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Ofisa Mkuu wa Wateja wadogo Benki ya NMB, Abdulmajid Nsekela akishuhudia.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker (katikati) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari namna ambavyo Hospitali Binafsi ziotakavyonufaika na mikopo nafuu ambayo itatolewa kwa wahitaji mara baada ya kupata mafunzo na ushauri toka kwa mfuko wa MCF. Kulia ni Kaimu Ofisa Mkuu wa Wateja wadogo Benki ya NMB, Abdulmajid Nsekela na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa MCF, Bi. Dolfing- Vogelenzang. Mikopo inayotolewa itaanzia USD 15,000/- hadi USD 1,000,000/- kulingana na mahitaji ya kituo au hospitali yenyewe.

Kaimu Ofisa Mkuu wa Wateja wadogo Benki ya NMB, Abdulmajid Nsekela kizungumza na wanahabari kuelezea namna hospitali binafsi zinavyoweza kunufaika na mkataba wao na MCF. Kushoto akifuatilia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker. Mikopo inayotolewa itaanzia USD 15,000/- hadi USD 1,000,000/- kulingana na mahitaji ya kituo au hospitali yenyewe.

Maofisa wa Benki ya NMB na Mfuko wa MCF wakibadilishana mawazo nje ya ukumbi wa mikutano wa NMB baada ya kumaliza kusaini hati za makubaliano.  Katika utaratibu huo NMB itatoa mkopo kuanzia USD 15,000/- hadi USD 1,000,000/- kulingana na mahitaji ya kituo au hospitali yenyewe.


No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...