Thursday, June 23, 2016

Ubia wa TTCL na Bharti Airtel Wafikia Kikomo

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (wa kwanza kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Profesa Tolly Mbwete (katikati) hati ya mauzo ya hisa asilimia 35 za Kampuni ya Bharti Airtel Afrika. Serikali imezinunua rasmi hisa za kampuni hiyo ndani ya TTCL ambapo leo wamesaini mkataba wa mauziano wa hisa hizo. Kulia ni  Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria akishuhudia.

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (kushoto waliokaa) akitiliana saini na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria (mwenye tai nyekundu) kwenye hafla ya kusaini mkataba wa mauziano. Serikali leo imezinunua rasmi hisa asilimia 35 za kampuni ya Bharti Airtel Afrika ndani ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL). Nyuma waliosimama ni viongozi mbalimbali walioshuhudia tukio hilo.
Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (mwenye tai ya bluu) akionesha hati ya mauziano ya hisa. Serikali leo imezinunua rasmi hisa asilimia 35 za kampuni ya Bharti Airtel Afrika ndani ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), ambapo sasa inakuwa ikiimiliki TTCL kwa asilimia 100. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria (mwenye tai nyekundu) akiwa kwenye hafla ya kusaini mkataba wa mauziano hayo.  Nyuma waliosimama ni viongozi mbalimbali wa TTCL na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano walioshuhudia tukio hilo.

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (kushoto) akibadilisha hati ya mkataba wa mauziano ya hisa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria. Wanaoshuhudia ni viongozi mbalimbali walioshuhudia tukio hilo.

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (mwenye tai ya bluu) akionesha hati ya mauziano ya hisa. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria (mwenye tai nyekundu). Kulia ni Ofisa Mkuu Mdhibiti wa Kampuni ya Bhart Airtel Afrika, Daddy Mukadi akiwa kwenye hafla hiyo.  

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (katikati) akizungumza katika hafla ya kutiliana saini ya mauziano ya hisa. Serikali leo imezinunua rasmi hisa za Kampuni ya Bharti Airtel Afrika. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Maria Sasabo akiwa katika hafla hiyo na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura (wa kwanza kulia). 

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (kulia) akijadiliana jambo na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) kwenye hafla ya kutiliana saini ya mauzo ya hisa za kampuni ya Bharti Airtel Afrika leo Dar es Salaam.

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (kushoto) akijadiliana jambo na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria kwenye hafla ya kutiliana saini ya mauzo ya hisa asilimia 35 za kampuni ya Bharti Airtel leo Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...