Sunday, June 12, 2016

Serikali Kuwatumbua Wanaopokea Rushwa Kwenye Mizani

Muonekano wa ujenzi wa kituo cha Mzani Itigi, kinachojengwa katika barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya, mkoani Singida.

SERIKALI imesema itachuku hatua kali ikiwemo kumfukiza kazi na kumfikisha mahakamani mfanyakazi wa Mizani atakayebainika anajihusisha na vitendo vya kupokea rushwa ili kuruhusu magari kupita bila kupimwa uzito.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Joseph Nyamhanga wakati alipokagua huduma za upimaji uzito wa Magari katika Mzani wa Njuki Mkoani Singida. Alisema hadi sasa kuna baadhi ya wafanyakazi wa Mizani wameachishwa kazi kutokana na kujihusisha na vitendo vya kupokea rushwa kutoka kwa madereva wa magari ya Mizigo na abiria.

“Hatutasita kuchukua hatua kwa mfanyakazi yeyote atakayejihusisha na vitendo vya rushwa, hatua kali tutachukua dhidi yake ikiwemmo kumfikisha mahakamani”. Amesema Eng. Nyamhanga.

Badala yake Eng. Nyamhanga amewataka wafanyakazi wote wa Mizani nchini kufanya kazi kwa uadilifu kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa Mizani ili kuweza kuleta ufanisi katika vituo vya kazi.

Pia amewataka madereva wa magari na abiria nchini kushirikiana na Wizara hiyo kwa kutoa taarifa za Wafanyakazi wa Mizani wanaowaomba rushwa ili kuweza kuondoa kero hiyo kwa wananchi wanaotumia hudum za Mizani nchini. Vile levile amewaasa madereva wa magari ya mizigo kutozidisha uzito wa mizigo kwenye magari ili kuepusha uharibifu wa barabara ambazo hujengwa kwa kutumia kodi za wananchi.

“Madereva mnawajibu wa kulinda barabara hizi kwa kutozidisha uzito wa mizigo kwenye magari yenu ili kuziwezesha barabara zetu zidumu kwa muda mrefu”. Amesisitiza Eng. Nyamhanga.

Aidha, Eng. Nyamhanga amesema Wafanyabiashara na madereva wa magari makubwa ya mizigo yaendayo nje ya nchi kuchangamkia fursa ya kuwapo kwa stika maalum za magari hayo kwani kutapunguza idadi ya vizuizi vya upimaji wa uzito na hivyo kuharakisha safari zao.

Naye Msimizi wa Mzani wa Njuki Mnanka Chile amewaomba madereva wa magari kuzingatia sheria na kanuni za alama za barabarabi na kuwa makini pindi wanapokaribia seheme za Mizani ya kupimia uzito wa Magari.

Katibu Mkuu Eng. Josph Nyamhanga yupo katika ziara ya kukagua Miradi ya Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, Vivuko na huduma za Mizani katika Mikoa ya Dodoma, Manyara Singida na Mara.

Imetolewa na kitenga cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...