Tuesday, July 5, 2016

BINTI WA MCHUNGAJI KULOLA APATA MWENZA.

Bwana Harusi, Richard Jeremiah Gwapulukwa (kushoto) wa Kasamwa mkoani Geita, amefunga ndoa na Happness Daniel Kulola (kulia) ambae ni binti wa Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza.

Ndoa imefungwa katika Kanisa hilo  na Mchungaji Paul Thomas Bagaka ambae pia ni msajili wa ndoa Manispaa ya Ilemela. Hafla ya ndoa hiyo inafanyika katika Ukumbi wa New Sun City Hotel Jijini Mwanza.


Maharusi wakiingia Kanisani kwa ajili ya Kufunga ndoa 
Maharusi wakisalimia. Pembeni ni wasimamizi
Mchungaji Paul Thomas Bagaka ambae pia ni msajili wa ndoa Manispaa ya Ilemela, akitoa somo la ndoa kabla ya kuwafungisha maharusi ndoa
Mchungaji Paul Thomas Bagaka awakiwafungisha maharusi ndoa
Bwana harusi akimvalisha bibi harusi pete ya ndoa
Bibi harusi akimvalisha bwana harusi pete ya ndoa
Maharusi wakiombewa na viongozi wa dini pamoja na wazazi
Maharusi pamoja na wasimamizi
Kutoka kulia ni Mchungaji  Dkt.Daniel Moses Kulola, Mama Mchungaji, Mercy Daniel Kulola, Mama mzazi na mchungaji na viongozi wa kanisa.
Brighters wakiingia ukumbini
Ndoa ilishuhudiwa na ndugu, jamaa na marafiki wakiwemo waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya.
Na BMG


No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...