Monday, August 24, 2015

PSPF Yakabidhi Magodoro 118 UDSM


 Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam, (Anayeshughulikia masuala ya Utawala), Profesa David Mfinanga, (Watatu kushoto), akipeana mikono na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (watatu kulia), wakati akipokea msaada wa magodoro 118 yaliyotolea wan Mfuko huo kwenye hafla fupi iliyofanyika chuon I hapo, Agosti 24, 2015. Magodoro hayo ni kwa ajili ya wanafunzi walioathiriwa na mogto uliozuka kwenye bweni kitalu B kule hosteli za Mabibo, Aprili mwaka huu 2015.

NA K-VIS MEDIA
MFUKO wa Pensheni wa PSPF, leo Agosti 24, 2015, umekipatia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, UDSM, magodoro 118 ili kusaidia huduma ya malazi kwa wanachuo walioathirika kutokana na bweni lao kuungua moto kwenye hosteli ya chuo hicho Mabibo jijini Dar es Salaam Aprili mwaka huu.
Akikabidhi msaada huo kwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, (Anayeshughulikia masuala ya Utawala), Profesa David A. Mfinanga, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, amesema, PSPF, iliguswa na ajali hiyo ya moto ambayo iliyotokea  kwenye bweni kitalu namba B na kusababisha mamia ya wanachuo kupoteza mali zao.
“Kwa kutambua kuwa wanachuo ni sehemu ya jamii ya Watanzania, na pia ni wanachama watarajiwa wa Mfuko, tumeona tuchangia sehemu ya vifaa ili wanafunzi waweze kurejean katika hali yao ya kawaida.” Alisema Njaidi.
Akitoa shukrani zake, kwa niaba ya Chuo, Profesa Mfinanga aliishukuru PSPF, kwa msaada huo ambao kwa hakika umesaidia pakubwa, kwani magodoro hayo yatapelekwa kwa walengwa na hivyo kusaidia kuwapunguzia machungu waliyoyapata kutokana na kuunguliwa vifaa vyao.
Kwa mujibu wa viongozi wa Chuo hicho, jingo hilo lilikuwa ,linakaliwa na wanachuo 788, wakati linawaka moto.

 Profesa mfinanga (wapili kushoto), akitoa shukrani kwa niaba ya chuo mbele ya maafisa wa PSPF,  viongozi wa wanachuo na wafanyakazi wa chuo hicho wakati wa hafla hiyo
 Afisa Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (kushoto), akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, baada ya kukabidhi msaada huo, Agosti 24, 2015
 Paulina Mabuga, mfanyakazi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaa, (wapili kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo. Wakwanza kushoto ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi, Denis Bashulula
 Profesa Mfinanga na Njaidi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali ya wanafunzi UDSM
Mfanyakazi wa UDSM, akipita jirani na magodoro hayo


No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...