Tuesday, November 19, 2013

Sherehe ya Beatrice Mroki Siku Alipopata Sakramenti ya Kipaimara Jijini Dar es Salaam

Novemba 17, 2013 ilikuwa siku ya furaha sana kwa Beatrice Mroki (kushoto) kwa kupata sakramenti yake ya Kipaimara baada ya kuhitimu mafunzo ya miaka miwili katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Ukonga jijini Dar es Salaam. Pichani ni Beatrice akigonganisha glasi na msimamizi wake Neema Steven wakati wa tafrija maalum ya kumpongeza iliyofanyika katika ukumbi wa Samunge Ukonga Mazizini.

 Hapa ilikuwa Kanisani wakisubiri kupokea Kipaimara katika KKKT Ukonga.

 Baada ya Kipaimara baba na mama yake Beatrice wakilamba picha na Binti yao.

 Nasisi tulijipongeza kwa malezi bora Mungu aliyotujalia.

 Bibi zake Beatrice wakijipongeza na kumtakia heri Mjukuu wao.

 Beatrice na wapambe wake...

Pongezi kutoka kwa wazazi...

 Dada Kilave akimpongeza mdogo wake

 Kikundi cha Ligimilo wakicheza kwaito...

 Keki ilikuwa hiviii ...

 na ilikatwa hivi....

 Ikaliwa hivi... Hapa Beatrice akimlisha mdogo wake Glory.


 Father Kidevu wakati wa zawadi alimpa gwala binti yake

 Muongezaji maarufu wa filamu za Kibongo Leah Mwendamseke nae alikuwepo.


 Ligimilo wakitangaza zawadi yao..

 Weee...!! Tulia nami nimsaidie baba leo...Glory Mroki akimfotoa dadayake picha.

 Kazawadi haka jamani... siku moja nitavaa shati lake.

 Huko jikoi mambo yalikuwa hivi

 Mwisho lilishuka sebene kali kutoka kila aina ya muziki kuanzia injili hadi katika kiduku namna hii.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...