Saturday, March 17, 2018

WANAWAKE WAASWA KUCHANGAMANA KUTENGENEZA FURSA ZA KIUCHUMI


 Mkurugenzi wa Taasisi ya I-learn East Afrika, Noelah Bomani (Kulia) akimkabidhi tuzo Mwanamke aliyefanya vizuri na kuwa kivutio katika mafanikio yake katika kipindi cha mwaka 2017/2018, Joyce Ibengwe Nangai ambaye ni Meneja Mawasiliano na Masoko  wa Chama cha Waajiri  Tanzania (ATE). (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs)
Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifatilia mada.
Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifatilia mada.
Mawenyekiti wa Chemba ya Wajasiriamali Wanawake Tanzania (TWCC) Jacqueline Maleko akizungumza kuwaelezea  uzoefu aliopitia na kuwasisitizia umuhimu wa kuchangaman ili waweze kutengeza fursa za kiuchumi hata kijamii wakati wa usiku wa Wanawake na tunzo kwa Mwanamke aliyefanikiwa kwa mwaka 2018 iliyoandaliwa na Tasisi ya Shangwe ambapo wanawake kutoka sehemu mbalimbali walikutana na kuzungumza mambo ya ujasilimali na namna ya kuvuka kutoka hatua moja hadi nyingine.
Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa.
Meneja Bima ya magari kutoka shirika la Bima ya Taifa (NIC) Emakulata Mwaitege, akizungumza umuhimu wa Wanawake kujiwekea bima katika biashara zao na maisha yao hili waweze kusimama tena pindi majanga yanapowakuta.
Muigizaji na  Msanii waTabasam PR Consultant, Regina Beraldo Kihwele akitumbuiza  katika kongamano hilo.
Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa.
Mshereheshaji wa Kongamano hilo, Angela Kileo akiwajibika katika hafla hiyo. 
 Meneja mafao kutoka mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF, Rosemary Mchagula akileza umuhimu wa wanawake kujiunga na mfuko huo kutokana na mafao yanayotolewa katika kuwasaidi kwa kulitaja fao la uzazi. Kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Shangwe Event, Deus Ntukamanzina.
Mmoja ya Wanawake walioshiriki katika kongamano hilo  akichangia katika mada zilizokuwa zkitolewa kwenye kongamano hilo.
Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifatilia matukio katika kongamano hilo.
Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa.
Mmoja ya Wanawake walioshiriki katika kongamano hilo  akichangia katika mada zilizokuwa zkitolewa kwenye kongamano hilo.
Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa. Kulia ni wazazi wa Afisa Mtendaji wa Shangwe Events, Deogratiasi Ntukamzina na Mke wake (wa pili kulia) 
Afisa Masoko wa Kituo Cha Uwekezaji nchini(TIC), Latifa Kigoda akileza ni namna gani wanawake wanaweza wakaungana na kuwa wawekezaji wakubw akatika mapinduzi haya ya uchumi wa Viwanda nchini.
 Mmoja ya Wanawake walioshiriki katika kongamano hilo kutoka TIB, Lisa Zavalla akichangia juu ya umuhimu wa wanawake kujikwamua kiuchumi katika mapinduzi ya uchumi wa Viwanda.
 Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifuatilia mada mbalimbali kwenye kongamano hilo.
 Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifuatilia mada mbalimbali kwenye kongamano hilo. Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Mamlaka ya Uchui na Uwekezaji Nchini (EPZA) Grace Lemunge . 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya I-learn East Afrika, Noela Bomani akieleza umuhimu wa wanawake kuchangamana na watu mbalimbali hili waweze kujikwamua kiuchumi kuliko kukaa sehemu moja kusubiri fursa ziwafate.
Sehemu ya Wanawake waliohudhuria kongamano hilo wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa.
Mwanasaikolojia na Mshauri wa masuala ya familia, Sadaka Said, akieleza umuhimu wa mwanamke kuambatana na mabinti zao katika maisha hili kuwajenga kwa ajili ya kesho yao kuliko kuwaacha nyumbani.
Afisa Mtendaji mkuu wa Shangwe  Event, Deus Ntukamanzina akizungumza na  Wanawake waliofika katika hafla hiyo na kuwashukuru kwani kukutana kwao ndio mwanzo wa wao kupiga hatua kubwa zaidi
Afisa Mtendaji Mkuu wa Secrets Lingerie, Fatna Tambwe (kushoto) na Afisa Masoko wa Kimtandao wa Mult-Choice Tanzania Grace Mgaya wakifuatilia mada katika konganano hilo. 

Mobile Week Kutoa Simu za Kisasa kwa Bei Che!

Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (kati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Simu (Mobile Week) itakayofanyika Machi 24 - 30 na kutoa ofa kabambe ya punguzo la bei kwa manunuzi simu za kisasa za mkononi kupitia tovuti ya Jumia (www.jumia.co.tz). Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Jumia, Zadok Prescott pamoja na Meneja Uhusiano wa Tecno, Eric Mkomoye (kushoto).

Mkurugenzi Mtendaji wa Jumia, Zadok Prescott (wa pili kulia) 


akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Simu (Mobile Week) itakayofanyika Machi 24 - 30 na kutoa ofa kabambe ya punguzo la bei kwa manunuzi simu za kisasa za mkononi kupitia tovuti ya Jumia (www.jumia.co.tz). Waliombatana naye ni Mkurugenzi wa Samsung Tanzania, Suleiman Mohammed (wa kwanza kulia),  Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (wa pili kushoto) pamoja na Meneja Uhusiano wa Tecno, Eric Mkomoye (kushoto).

Mkurugenzi wa Samsung Tanzania, Suleiman Mohammed (wa kwanza kulia)  

Meneja Uhusiano wa Tecno, Eric Mkomoye (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Simu (Mobile Week) itakayofanyika Machi 24 - 30 na kutoa ofa kabambe ya punguzo la bei kwa manunuzi simu za kisasa za mkononi kupitia tovuti ya Jumia (www.jumia.co.tz). 


WATEJA watafurahia punguzo kubwa la bei hadi 60% kwa simu za kisasa (smartphone) kupitia Jumia Mobile Week (wiki ya simu) itakayofanyika kwenye mtandao wa manunuzi ya bidhaa wa Jumia (www.jumia.co.tz). Pamoja na punguzo hili kubwa la bei, simu zote za kisasa zitakazouzwa katika promosheni hii zitakuwa na ofa ya hadi GB 18 ya intaneti bure kutoka kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali ya Tigo Tanzania.

Katika uzinduzi wa gulio hilo la simu kwa njia ya mtandao, Jumia pia walizindua Ripoti ya Sekta ya Simu za Mkononi Tanzania inayoonesha kuwa asilimia 83% ya Watanzania walitembelea mtandao wa Jumia kupitia simu zao za mkononi, ikilinganishwa na asilimia 17% tu waliotumia kompyuta. Matokeo haya yanadhihirisha kuwa Watanzania wengi wamevuka kigezo cha matumizi ya kompyuta na badala yake wanatumia teknologia ya  simu za mkononi kutekeleza shughuli zao za kila siku.

Akitangaza ushirikiano huo kabambe jijini Dar es Salaam, Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael alisema kuwa Mobile Week itakayoanza 24 – 30 Machi ndio muda muafaka zaidi wa kununua simu ya kisasa kwa sababu simu zote zitapatikana kwa bei nafuu zaidi ambazo hazijawahi kutokea nchini, huku kila simu ikiwa na ofa ya hadi GB 18 za intaneti kutoka Tigo.

‘Tigo inaongoza katika mageuzi ya maisha ya kidigitali. Lengo letu ni kuongeza idadi ya watumiaji wa simu za kisasa nchini huku tukihakikisha kuwa wateja wetu wote wanapata huduma bora, za uhakika za mtandao. Huduma bora za kidigitali zinaanza na vifaa  bora, ndio maana ushirikiano wetu na Jumia utahakikisha kuwa kila mmoja anapata simu mpya ya kisasa pamoja na ofa za intaneti zitakazomwezesha mtumiaji kuwa sehemu ya maisha ya kidigitali,’ alisema.

Akifafanua jinsi ya kupata ofa hizi za simu, Mkurugenzi Mtendaji wa Jumia Tanzania, Zadok Prescott aliwashauri wateja kutembelea tovuti ya www.jumia.co.tz ambapo watapata aina mbali mbali za simu kutoka kwa wauzaji mbali mbali. Baada ya hapo wanaweza kuchagua aina ya simu wanayoipenda na kutoa maelekezo ya sehemu ambapo wangependa kuletewa simu yenyewe na watoa huduma wa Jumia. Wasiokuwa na huduma za mtandao wanaweza kupiga simu namba 0800 710024 bila gharama yoyote ili kutoa maombi ya simu wanayoitaka.
‘Nawahamasisha nyote mchangamkie ofa kabambe za simu zitakazopatikana katika mtandao wa Jumia katika kipindi hiki cha Mobile Week. Tunafurahia kuleta pamoja baadhi ya kampuni kubwa zaidi za simu duniani kama vile Tigo,  Samsung, Tecno na Infinix kushiriki katika gulio hili la kila mwaka. Kwa pamoja tumefanikiwa kuwaletea ofa ambazo hazijawahi kutokea kwa simu za kisasa, ikiwemo simu zenye uwezo wa 3G zitakazopatikana kuanzia TZS 50,000/- pekee na zile za 4G zitakazopatikana kwa chini ya TZS 150,000/- tu,’ Zadok alisema.

‘Wateja wana uhuru wa kuja kuchukua simu zao kutoka katika ofisi za Jumia ama wanaweza kuletewa simu zao mahali popote walipo. Malipo kwa ajili ya simu yatafanyika kwa njia ya Tigo Pesa au kwa pesa taslim mara tu baada ya mteja kupokea simu aliyoagiza na sio vinginevyo. Hii inaondoa hofu ya  kutapeliwa,’ Zadok alimaliza.

Ukuaji wa simu za kisasa (smartphone) unatoa fursa kubwa kwa matumizi ya mtandao kutoa huduma mbali mbali kwa Watanzania kupitia mifumo kama Jumia. Hivi karibuni idadi ya watumiaji wa simu za mkononi nchini ilifikia watu milioni 40, huku idadi ya wanaotumia mtandao ifikia watu 23 milioni.

“Idadi ya watu wanaotumia simu za kisasa inakua kwa kasi siku hadi siku. Hii ni hatua muhimu katika maendeleo ya simu za mkononi, ila upatikanaji wa vifaa vya kisasa bado ni changamoto kubwa. Jumia imejikita kuhakikisha kuwa Watanzania wote wanapata simu za kisasa, hasa katika kipindi hiki cha Mobile Week,” Zadok alibainisha



Friday, March 16, 2018

Serikali yajipanga kupokea mradi wa Global Learning XPRIZE


  Serikali imesema inajiandaa kuupokea mradi wa ‘Global Learning XPRIZE’ unaowawezesha watoto walio nje ya mfumo rasmi kujifunza stadi za msingi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kupitia Michezo iliyowekwa kwenye tableti, kutoka kwa wadau wanaoufadhili baada ya kumalizika muda wa majaribio. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi kutoka TAMISEMI anayeshughulikia elimu nje ya mfumo rasmi na Elimu ya Watu Wazima, Odilia Mushi wakati akizungumza katika mkutano uliokutanisha wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), na taasisi mbalimbali za serikali.
Mkurugenzi Msaidizi kutoka TAMISEMI anayeshughulikia elimu nje ya mfumo rasmi na Elimu ya Watu Wazima, Odilia Mushi akizungumza kuhusu maandalizi ya serikali kuupokea mradi wa Global Learning XPRIZE.
Kama serikali mradi unapomalizika tunaangalia namna ya kuuendeleza. Tutaendelea kushirikiana na halmashauri zetu zilizoko kwenye mradi wauone kama ni wa kwao na kwamba badala ya watoto kuzurura mitaani wanaendelea kujifunza,” amesema Mushi na kuongeza. “Tunaagiza wale wahusika, wadau wa elimu katika ngazi zote za kijiji hadi mkoa wa Tanga waone kama hiki kilicholetwa kwetu ni zawadi,na ni lazima kuuendeleza ili kupunguza watoto walioko nje ya mfumo rasmi; kwa maana hiyo inatakiwa tuwe na ushirikiano kuona changamoto baada ya huu mradi kumalizika ili kuzifanyia kazi.”
Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo akizungumza kuhusu mradi wa Global Learning XPRIZE.
Akielezea utekelezaji wa mradi huo tangu ulipoanza na ulipofikia, Afisa Msaidizi wa Mradi kutoka UNESCO, amesema hadi sasa watoto zaidi ya 2000 kutoka vitongoji 141 katika wilaya 6 za mkoa wa Tanga wamenufaika na mradi huo. “Baada ya miezi 15 ya mradi kukamilika, mradi utakabidhiwa kwa serikali ili kuendelea kuusimamia. , ambapo tumekutana leo Tarehe 13/3/2018 na wawakilishi kutoka Baraza la Mitihani la Tanzania (BMT) , Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na TAMISEMI ili kuweza kuangalia ni jinsi gani watoto walio katika mradi wataingia katika mfumo rasmi katika ngazi husika,” amesema.
Wadau mbalimbali wakichangia katika mkutano uliokutanisha wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), na taasisi mbalimbali za serikali kuhusu mradi wa Global Learning XPRIZE.

Washiriki wa mkutano uliokutanisha wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), na taasisi mbalimbali za serikali kuhusu mradi wa Global Learning XPRIZE.

Tuesday, February 27, 2018

Shirika la TTCL lazinduwa huduma ya 'Fiber Connect Bundle'

Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Corporation, Bw. Waziri Kindamba akizungumza katika uzinduzi huo.


SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL CORPORATION) limezinduwa rasmi huduma mpya inayojulikana kama 'Fiber Connect Bundle' inayokwenda pamoja na kauli mbiu ya "Rudi nyumbani, kumenoga" kuchagiza uzinduzi huo.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Corporation, Bw. Waziri Kindamba alisema huduma hiyo ni mwendelezo wa ubunifu wa kampuni ya kizalendo katika kuwapatia Watanzania huduma za kipekee, nafuu na zenye ubora wa hali ya juu.

Bw. Kindamba alisema TTCL Corporation imedhamiria kuwafuata wateja nyumbani na kufanya mapinduzi makubwa ya kimawasiliano hasa ya mtandao wa intanenti yenye kasi ya juu.

Alisema kupitia huduma hiyo mpya ya Fiber Connect Bundle, wateja wao watapata huduma nne kwa pamoja zikiwa na unafuu mkubwa wa gharama na ubora wa hali ya juu ukilinganisha na mitandao mingine ya simu.

Bw. Kindamba amefafanua huduma kwa kuanzia wanatarajia kuzifikia nyumba 500 katika maeneo ya Mikocheni na nyumba nyingine 500 katika eneo la Mbezi Beach jijini Dar es Salaam pamoja na nyumba 200 eneo la Medeli mkoani Dodoma.

Aidha aliongeza kuwa baada ya hapo wataendelea na maeneo mengine kwani lengo lao ni kuhakikisha kila mahali katika nchi yetu kunakuwa na huduma za mawasiliano ya Shirika hilo hasa kwa kuzingatia wao ndio wanaousimamia mkongo wa Taifa wa mawasilano.

Kindamba amesema kupitia kifurushi cha Fiber Connect, mteja wao atanufaika na huduma mbalimbali ikiwamo ya  kupata intanenti yenye kasi isiyo na kikomo (Unlimited). Pia mteja atapata huduma ya simu za sauti kwa simu za mezani na simu card ambayo ataitumia kwenye simu yake ya mkononi na kupata huduma ya Intanenti sawa na simu ile anayopata katika simu ya mezani.

Ameongeza kuwa mteja wao pia atapata huduma za Wireless Service (WIFI) katika nyumba yake ambapo vifaa vyote vinavyotumia teknolojia ya intaneti vitaunganishwa  ili kutumia kutumia huduma hiyo.

Ametoa mfano kuwa huduma ambayo wameizundua mteja anaweza kuunganisha kwenye Smart Tv, Tablets na kompyuta mpakato.Pia mteja atapatiwa vifaa vyote bure na uhakika wa huduma za baada (After Sell Services) endapo itahitajika.

Amesema kuwa wamejipanga kuhakikisha wanaendelea kutoa huduma bora kwa ajili ya Watanzania ambao kimsingi shirika hilo ni mali yao na wanatakiwa kuunga mkono jitihada hizo.

“Tumeendelea kujipanga ili kufikia malengo yetu ambayo kimsingi ni kuwatumikia Watanzania kwa kiwango bora katika eneo la mawasiliano na kwa gharama nafuu,” amesema Bw. Kindamba.

Akizungumzia shirika hilo, Kindamba amesema, Februari moja mwaka 2018, Shirika la Mawasiliano Tanzania lilizaliwa kwa sheria ya Shirika la Mawasiliano Tanzania Na. 12 mwaka 2017. Amesema kwa sasa shirika hilo limechukua sura  ya iliyokuwa Kampuni ya Simu Tanzania( TTCL),  ambayo shughuli zake ziliisha Januari  31 mwaka 2018.

Amemshukuru Rais, Dk. John Magufuli kwa kuona umuhimu wa kuwa na Shirika madhubuti la mawasiliano la Taifa kwa maslahi mapana ya Taifa. Pia amemshukuru kwa kuendelea kuonesha imani kubwa kwa uongozi wao.

WAHUDUMIENI WANANCHI BILA YA UBAGUZI - MAJALIWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia ngoma ya kikundi cha Teleza wakati alipo wasili, Wilayani Newala, akiwa kwenye ziara yake ya kikazi ya siku tatu, Mkoani Mtwara  Februari 27, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa umma wawatumikie wananchi kwa uweledi na ustadi bila ya ubaguzi wa aina yoyote. Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo jana (Jumatatu, Februari 26, 2018) wakati akizungumza na watumishi wa wilaya za Masasi na Nanyumbu kwa nyakati tofauti.

Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Mtwara kwa ziara ya kikazi aliwasisitiza watumishi wa umma kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Alisema Rais Dkt. John Magufuli amesisitiza watumishi wa umma wawatumikie wananchi bila ya ubaguzi wowote pamoja na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

“Watumishi wa umma lazima mtambue kwamba msimamo wa Serikali ni kuwahudumia wananchi bila ya ubaguzi wa kidini, kiitikadi na kipato.”

Waziri Mkuu alisema ni vyema watumishi hao kuanza kujitathmini kwa sababu Serikali haitowavumilia watumishi watakaoshindwa kuwajibika kwa wananchi.

Pia aliwataka watendaji hao kuacha urasimu na wahakikishe kila fedha iliyotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inatumika kama zilivyoelekezwa.

Waziri Mkuu aliwaagiza watendaji hao wawe na mpango wa kuwatembelea wananchi kwa ajili ya kusikiliza kero zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi. 

Benki ya NMB yafungua tawi jipya Ruaha, Iringa

Mkuu wa mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi 
la NMB Ruaha Mkoani Iringa. Tawi hili litakua ni tawi linafikisha idadi ya matawi 214 ya NMB nchi 
Nzima. Kushoto ni Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini, Badru Idd na Mkuu wa Kitengo cha wateja wadogo na wakati, Abdulmajid Nsekela (kulia) wakishuhudia tukio hili lililofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Iringa

Mkuu wa mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi 
la NMB Ruaha Mkoani Iringa. Tawi hili litakua ni tawi linafikisha idadi ya matawi 214 ya NMB nchi 
Nzima. Kushoto ni Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini, Badru Idd na Mkuu wa Kitengo cha wateja wadogo na wakati, Abdulmajid Nsekela (kulia) wakishuhudia tukio hili lililofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Iringa

Mkuu wa mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi 
la NMB Ruaha Mkoani Iringa. Tawi hili litakua ni tawi linafikisha idadi ya matawi 214 ya NMB nchi 
Nzima. Kushoto ni Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini, Badru Idd na Mkuu wa Kitengo cha wateja wadogo na wakati, Abdulmajid Nsekela (kulia) wakishuhudia tukio hili lililofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Iringa


BENKI ya NMB Tanzania imezindua tawi jipya Ruaha ambalo limeanzishwa kwa lengo la kusogeza
huduma za kifedha karibu zaidi na wananchi wa mkoa wa Iringa.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tawi hilo, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa
Kati wa NMB Bw. Abdulmajid Nsekela alisema,” Benki ya NMB imeendelea kuwa benki yenye
mtandao mpana zaidi wa matawi na ATM; tawi hili likiwa ni la 214 na ATM zaidi ya 800 nchi
nzima huku ikiwa na mawakala wanaotoa huduma za NMB zaidi ya 4000 nchi nzima huku ikijivunia wateja wake zaidi ya milioni 3.

“Mafanikio haya yasingeelezwa leo kama si kuaminiwa na wateja wetu ambao miongoni mwao ni
wana Ruaha na Iringa kwa ujumla kuwa benki wanayoipendelea zaidi na hivyo kuwa ni benki
yenye mafanikio makubwa zaidi nchini.”

Pamoja na ufunguzi wa tawi hilo, pia benki ya NMB ilitoa msaada wa milioni 5 ambazo zitaelekezwa katika sekta ya afya na elimu, ambapo Nsekela aliitaka serikali kusema ni maeneo gani ingependa pesa hiyo itumika.

TENMET kushirikiana na Equality Now kupaza sauti za watoto


Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT), Bi. Cathleen Sekwao (kulia) akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa maonesho ya sauti za watoto juu ya changamoto anuai za ukatili zinazowakabili watoto, maonesho hayo yameandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT) kwa kushirikiana na taasisi ya Equality Now.

Meneja Kampeni wa Taasisi ya Equality Now, Bi. Florence Mashio akizungumza kuhusu unyanyasaji wa watoto hasa kwa mtoto wa kike pamoja na namna ya kuupinga ukatili huo wakati wa maonesho ya  ya sauti za watoto juu ya changamoto anuai za ukatilizinazowakabili watoto lililofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

MTANDAO wa Elimu Tanzania (TenMeT) na taasisi ya Equality Now imekubaliana kufanyakazi kwa pamoja kuhakikisha inapaza sauti za watoto juu ya changamoto mbalimbali za ukatili zinazowakabili hasa watoto wa kike.

Akizungumza jijini Dar es Salaam katika maonesho ya sauti za watoto juu ya changamoto anuai za ukatili zinazowakabili watoto, yalioshirikisha wanachama wa TenMet, Meneja Kampeni wa Equality Now, Bi. Florence Machio alisema matatizo yanayowakumba watoto katika nchi nyingi za afrika yanafanana hivyo kuna kila sababu ya kushirikiana kuyakabili.

Alisema vitendo vya unyanyasaji wa watoto vimekuwa vikiwakatili watoto ndoto zao na 
kurudisha nyuma Bara la Afrika kielimu, kwani wengi wamejikuta wanakatishwa masomo 
kutokana na ukatili wanaofanyiwa kama vile kutiwa mimba utotoni, kuozeshwa, vitendo vya 
ukeketaji na ubakaji dhidi yao.

"Matatizo yanayowakabili watoto nchini Tanzania hayana tofauti na yanayowakabili watoto katika mataifa mengine ya Afrika...hivyo tunapohimiza mabadiliko ya sera na sheria zisizowalinda watoto tuungane kwa pamoja bila kujali unatoka taifa gani," alisisitiza Bi. Machio.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT), Bi. Cathleen Sekwao akizungumza kabla ya kufungua majadiliano kwa wanachama alisema licha ya kushinikiza mabadiliko ya sera na sheria zinazoshindwa kuwalinda watoto sauti za mtoto mwenyewe hazina budi kupazwa ili zisikike kwa jamii nzima.

Aliwataka wajumbe wa mkusanyiko huo kutoka na suluhisho baada ya majadiliano ya pamoja ili kumsaidia mtoto kufikia malengo yake. Alisema wajumbe watapata muda wa kupitia sauti za baadhi ya watoto wakiwa katika changamoto zinazowakabili na kutoka na suluhisho la pamoja kumlinda mtoto.

Mkutano huo mbali na kushirikisha wanachama wa TenMeT ulihudhuriwa pia na wadau pamoja na wawakilishi wa Serikali kutoka idara husika. Equality Now inafanya kazi katika mataifa ya Sierra Leone, Gambia, Mauritania, Kenya, Uganda na Tanzania.


Mwezeshaji na Meneja Programu wa Mtandao wa Elimu Tanzania, (TenMet), Bw. Nicodemus Shauri Eatlawe akizungumza namna ya kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia hasa kwa mtoto wa kike.

Baadhi ya wadau wakiangalia mabango yenye ujumbe mbalimbali zinazohusu kupaza sauti kwa ukatili wa mtoto wakati wa maonesho ya sauti za watoto juu ya changamoto anuai za ukatilizinazowakabili watoto lililofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Afisa Programu wa TenMet, Bi. Alistidia Kamugisha (kulia) akichangia mada kwenye mkutano huo.

Baadhi ya wadau mbalimbali wakichangia mada wakati wa maonesho ya sauti za watoto juu ya changamoto anuai za ukatilizinazowakabili watoto lililofanyika leo Jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya wadau kutoka taasisi Binafsi na serikali wakiwa kwenye mkutano uliowakutanisha ili kuangalia namna ya kusaidia mtoto wa kike wakati wa maonesho ya sauti za watoto.

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...