Friday, March 30, 2018

MAONYESHO YA YST 2018 KUFANYIKA AGOSTIST 2018

Mwanzilishi Mwenza wa  Young Scientists Tanzania (YST) Dk. Gosbert Kamugisha (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu maonyesho ya Young Scientists Tanzania (YST) 2018 yatakayofanyika mwezi Agosti mwaka huu Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC) jijini Dar se Salaam. Wengine kutoka kushoto ni Patricia Mhondo kutoka Kampuni ya Shell Explorstion snd Production Tanzania Ltd (shell) na Joseph Clawry kutoka nchi ya Iland. 
Meza Kuu pamoja na wadhamini wa maonyesho hayo.
Mkurugenzi wa Karimjee Jinanjee Foundation (KJF), Yusuf Karimjee akizungumzia udhamini wao 
Patricia Mhondo kutoka Kampuni ya Shell Explorstion snd Production Tanzania Ltd (shell) akizungumza kwenye mkutano huo.
Joseph Clawry kutoka nchi ya Iland akizungumzia kazi za ubunifu na jinsi nchi yao inavyowawezesha wanafunzi waliofanya vizuri katika miradi yao.
Muonekano wa chumba cha mkutano huo.

Na Dotto Mwaibale

MAONYESHO ya Young Scientists Tanzania (YST) 2018 yatafanyika mwezi Agosti mwaka huu Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC) jijini Dar se Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Mwanzilishi Mwenza wa YST, Dk. Gosbert Kamugisha alisema maonesho hayo yatafanyika kuanzia tarehe moja hadi mbili mwezi huo.

"Wanafunzi wote wanaopenda kushiriki wanashauriwa kutuma kazi za miradi yao kwenda YST kabla ya tarehe 21 Aprili 2018" alisema Kamugisha.

Kamugisha alisema wanafunzi 200 watakaochaguliwa wataonyesha kazi za teknolojia na ugunduzi wa kisayansi kwenye onesho hilo la mwaka huu na kuwa na wanafunzi watakaochaguliwa watapewa mafunzo kutoka kwa washauri wa sayansi wa YST kuhusu namna ya kutengeneza kazi zao za kisayansi.

Alisema onesho hilo pamoja na mpango wa kuzitembelea shule na wanafunzi kuwapatia ushauri wa kisayansi vinawezeshwa na wadhamini wakuu wa YST ambao ni Shell Explorstion snd Production Tanzania Ltd (shell) na Karimjee Jinanjee Foundation (KJF)

"Tunapenda kuwashukuru wadhamini wetu tangu mwaka 2012. Mwaka huu wa 2018 KJF wameongeza kiwango cha udhamini na kuwa mmoja wapo wa wadhamini wakuu wa YST kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Alisema udhamini huo utaiwezesha programu ya YST kuwa endelevu na kuwawezesha vijana kufanya ubunifu na kufanya tafiti za kisayansi ili kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kamugusha aliongeza kuwa wanasayansi chipukizi wakaoshiriki onesho la YST mwaka huu kwa sasa wanaendelea kutengeneza kazi za miradi yao katika nyanja mbalimbali za kisayansi kama kemia, fizikia na hesabu, biolojia na ekolojia, saynsi ya jamii na teknolojia na kuwa kazi miradi nyingi zimejikita katika sekta ya afya,kilimo na usalama wa chakula, mawasiliano na usafirishaji, nishati,elimu, mazingira na mabadiliko ya tabia nchi.

Alisema wanafunzi watakajituma na kufanya ugunduzi mzuri watazawadiwa pesa taslimu, medali, vikombe na uimarishaji wa maktaba ya shule yao kama ambavyo wamefanya kwa miaka sita iliyopita KJF watawazadia wanafunzi wenye ugunduzi mzuri zaidi zawadi za udhamini wa masomo ya chuo kikuu ili kuwawezesha kusoma masomo ya sayansi na teknolojia katika ngazi ya chuo kikuu.

Wednesday, March 28, 2018

UBA Sustains Strong Performance with Growing Contribution and Market Share from Africa


  • Official%2BPicture%2Bof%2BGMD%2B-CEO%2Bof%2BUBA%2BPlc%2B%2B-Kennedy%2BUzoka

  • Declares Profit Before Tax of N105.3 billion 
  • Recommends N0.85 Total Final Dividend for the Year

United Bank for Africa Plc has announced its audited results for the financial year ended December 31, 2017, showing significant growth in the contribution and market share from its pan-African subsidiaries, among other positive trends in the financial performance.

The pan-African financial institution’s audited results showed that gross earnings grew substantially to N462 billion, up by 20 percent from N314 billion recorded in the corresponding period of 2017.

According to the report released to the Nigerian Stock Exchange on Friday, the Group delivered a strong 16% year-on-year growth in profit before tax of N105 billion, compared to N90.6 billion in the 2016 financial year. The Profit After Tax also leaped to N78.6 billion, an 8.8% year-on-year growth compared to N72.3 billion in 2016.

The Bank’s subsidiaries outside Nigeria contributed a third of the Group’s top-line and 45% of the profit for the year, a remarkable improvement from 31 percent contribution made by the ex-Nigeria offices in 2016. This, according to market analysts affirms the success of the Bank’s expansion strategy, with target of 50 percent contributions by 2020.

The Bank’s Operating Income grew to N326.6 billion, a 20.6 percent increase compared to N270.9 billion recorded in 2016. This, according to analysts, affirms the capacity of the Group to deliver strong performance through varying economic cycles and challenging business environment.

The audited results also showed that the Bank’s Total Assets peaked at N4.07 trillion, translating into 16.1 percent year-on-year growth from the figure of N3.50 trillion recorded as at 2016 financial year. In the 2017 financial year, the Bank’s Net loans achieved a prudent 9.7 percent growth at N1.65 trillion, while the customer deposits grew to N2.73 trillion, representing 10 percent YoY growth on N2.49 trillion recorded in 2016 financial year.

Reflecting a strong internal capital generation, the Bank’s shareholders’ fund also soared 18.2 percent to N529.4 billion in the 2017 financial year.

Subject to the approvals of the shareholders, the Board of UBA Plc proposed a final dividend of 65 kobo per every share of 50 kobo each. This final dividend proposal is in addition to the 20 kobo per share interim dividend paid after the audit of the 2017 half year financial statements, thus putting the total dividend for 2017 financial year at 85 kobo per share.

Commenting on the result, Kennedy Uzoka, the GMD/CEO, said: “the results, underlines the success of our strategy of expanding across Africa, diversifying revenues and capturing the broader business opportunities inherent in Africa’s growth. The results reinforce the sustainability of our business model and the capacity to deliver superior long-term return to shareholders, as the economic and business environment improve.”

“In 2017, we made strong progress in our strategic initiative of dominating transaction banking across all our countries of operation, gaining market share in all lines of our business. Even as the non-oil sectors of our largest country of operation, Nigeria, remained relatively weak, we still grew earnings by 20% to N462 billion, a third of which is attributable to non-funded income,” he further noted.  

Also speaking on UBA’s financial performance and position, the Group Chief Finance Officer(GCFO), Ugo Nwaghodoh said; “In a period of high interest rates, we achieved a relatively low 3.7% cost of funds. This operational efficiency reflects the benefit of our rich pool of stable savings and current account deposits. The net interest margin stabilized at 7%, even as yields on treasury assets dropped in the last quarter of 2017. Our core transaction banking offerings gained strong momentum, with income from these business lines growing by double digits.”

“We remain committed to our responsible approach to balance sheet management, with focus on growing risk asset and broader balance sheet in a profitable and prudent manner. Amidst a subdued Nigerian credit market, we grew our loan portfolio by 10%, leveraging our robust liquidity and capitalization to support good businesses through this challenging economic cycle. We closed the year with a Basel II capital adequacy ratio of 19% and a liquidity ratio of 50%, well ahead of 15% and 30% regulatory requirement respectively. Our disciplined approach to lending and broader risk management continues to uphold our asset quality.” 

Apart from the strong financial performance in 2017, UBA Group proved its leadership on the continent as the Banker Magazine crowned the Group, “African Bank of the Year 2017”.  To further demonstrate the group’s strength and dominance in the financial sector on the continent, four of UBA Group’s operations in Africa also led contenders in their respective countries to emerge the Best Bank of the Year 2017 in their respective markets. UBA Congo, UBA Tchad, UBA Gabon and UBA Senegal emerged the Best Bank of the Year in Congo, Tchad, Gabon and Senegal, reinforcing the strong franchise of the Group across its chosen markets in Africa.

United Bank for Africa Plc is a leading financial services group in sub-Saharan Africa, with presence in 19 African countries, as well as the United Kingdom, the United States of America and France.
From a single country operation founded in 1949 in Nigeria, Africa's largest economy, UBA has emerged as a pan-African provider of banking and other financial services, to c.10 million customers globally, through one of the most diverse service channels in sub-Sahara Africa; 632 business offices, 1,750 ATMs, some 13,500 PoS, and a robust online and mobile banking platform.
UBA was the first Nigerian bank to make an Initial Public Offering (IPO), following its listing on the NSE in1970. It was also the first Nigerian bank to issue Global Depository Receipts (GDRs). The shares of UBA are publicly traded on the Nigerian Stock Exchange (NSE) and the Bank has a well-diversified shareholder base, including foreign and local institutional investors as well as individual shareholders.

Friday, March 23, 2018

MAWAKALA TIGO PESA NCHI NZIMA WAENDELEA KUJISHINDIA ZAWADI

Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Simu za Mkononi ya Tigo, Kanda ya Kaskazin, Henry Kinabo akimkabidhi wakala wa Tigo Moshi mjini, Hassan, mfano wa Hundi ya Shilingi Milioni Mbili kwa kuibuka mshindi wa pili wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo kwa kanda ya Kaskazini. Promosheni hii inawahusu Mawakala zaidi ya 73000 wa Tigo Pesa nchi nzima huku zawadi za Shilingi za kitanzania Milioni 144 zikishindaniwa. 

Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Simu za Mkononi ya Tigo, Kanda ya Kaskazin, Henry Kinabo akimkabidhi wakala wa Tigo wilaya ya Same Real Stationary, mfano wa Hundi ya Shilingi Milioni tatu  kwa kuibuka mshindi wa kwanza wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo kwa kanda ya Kaskazini. Promosheni hii inawahusu Mawakala zaidi ya 73000 wa Tigo Pesa nchi nzima huku zawadi za Shilingi za kitanzania Milioni 144 
zikishindaniwa.


Meneja wa Tigo Kanda ya Ziwa, Gwamaka Mwakilembe (kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni ,mbili kwa Juliana Shilatu aliyeibuka kama wakala wa pili bora wa kanda ya Ziwa katika promosheni ya mawakala wa Tigo Pesa. Zawadi zenye thamani ya TZS 88 milioni zimetolewa na Tigo pesa kwa mawakala wake 73,000 nchini kote walioshiriki katika promosheni hiyo.

Meneja wa Tigo Mkoa Iringa Davis Kisamo (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi millioni 3/- kwa wakala wa Tigo Pesa, Gibson Chaula wa Songea mwishoni mwa wiki mkoani Iringa.

Meneja wa Tigo Mkoa Iringa Davis Kisamo (kushoto) na Meneja Mauzo wa Tigo Mkoa Iringa, Samuel Chanay (kulia) wakimkabidhi mfano wa hundi wakala wa Tigo pesa Asha Ramadhani aliyeshindia zawadi ya shilingi millioni 2/-  kwenye hafla iliyofanyika mkoani Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita.


Wednesday, March 21, 2018

Standard Chartered wachangia 1.1% ya GDP ya Tanzania

 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (katikati) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Makampuni na Taasisi za Fedha wa benki ya Standard Chartered, Jaffer Machano (kulia) mara baada ya kuwasili kwenye hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Kutoka kushoto ni Mwandishi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii, Rene Kim, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse pamoja na Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt (wa pili kulia).
 Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse (kushoto) akibadilishana mawazo na Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (katikati) pamoja na Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt (kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel akifurahi jambo na na Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo na Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Meza kuu kutoka kushoto ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse, mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna pamoja na Mwandishi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini, Rene Kim.
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel akizungumza na wafanyakazi wa benki ya Standard Chartered na wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
  Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (kushoto) kuzindua rasmi ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mwandishi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini, Rene Kim akifanya mchanganuo wa ripoti hiyo kabla ya kuzinduliwa kwa ripoti hiyo kwenye hafla iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt (kushoto) pamoja na Mkuu wa Makampuni na Taasisi za Fedha wa benki ya Standard Chartered, Jaffer Machano wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (wa pili kulia), Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse pamoja na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna wakizindua rasmi ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Makampuni na Taasisi za Fedha wa benki ya Standard Chartered, Jaffer Machano (kulia) na kushoto ni Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt.
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (wa pili kulia), Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse(wa pili kushoto), Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt (kushoto),  Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna (wa tatu kulia) pamoja na Mkuu wa Makampuni na Taasisi za Fedha wa benki ya Standard Chartered, Jaffer Machano (kulia) wakipiga makofi baada ya kuzinduliwa rasmi ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa wa benki ya Standard Chartered waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki hiyo kwa uchumi na jamii nchini, iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya wateja wa benki ya Standard Chartered, wafanyakazi wa benki hiyo, wanahabari pamoja na wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki hiyo kwa uchumi na jamii nchini, iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba (kushoto) akizungumza jambo na mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (kulia)alipokuwa akijiandaa kuondoka ukumbini hapo. Wengine ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse(wa pili kulia)pamoja na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna.
Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (wa tatu kulia) katika picha ya pamoja na meza kuu mara baada ya kuzindua ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.













Standard Chartered wachangia 1.1% ya GDP ya Tanzania

Na Mwandishi wetu

BENKI ya Standard Chartered imechangia asilimia 1.1 ya pato la taifa (GDP) sawa na kuwezesha huduma na bidhaa zenye thamani ya dola milioni 579.

Taarifa hiyo imetolewa wakati wa uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki hiyo kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena.

Alisema mchango wake pamoja na kusaidia upatikanaji wa kazi, biashara na ukuaji wa uchumi, imekuwa ikichangia maendeleo ya ukuaji wa sekta ya fedha katika miundombinu na utaalamu.

Katika uzinduzi huo uliofanywa na Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel, Benki hiyo imesema kwamba imewezesha nafasi za kazi za moja kwa moja na za msaada zipatazo 220,000 ikiwa ni sawa na asilimia moja ya watanzania wote walioajiriwa.

Kuhusiana na mchango wake katika uchumi wa Tanzania, ripoti inaonesha kwamba Standard Chartered Bank inahusika na ukuaji wa sekta ya biashara kwa asilimia 3.5 na katika viwanda ikiwa ni asilimia 3.7.

Pamoja na kutoa takwimu za mchango wake katika uchumi wa Tanzania, pia ripoti hiyo imeonesha namna bora ambapo benki inaweza kukuza mchango wake katika uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Benki imeshauri kufanya mambo kadhaa ikiwamo kuongeza shughuli zake za kuchochea ukuaji wa biashara kwa nchi za Afrika Mashariki na kujiimarisha katika soko hilo.

Kuelekeza nguvu zake katika sekta ya uzalishaji bidhaa kwa kusaidia kampuni za ndani kusonga mbele katika uzalishaji wa bidhaa na hivyo kuongeza kasi ya ukuaji wa kiuchumi.

Aidha imeelezwa benki hiyo ina fursa bado za kusaidia watu maskini, ambao ni lazima kuwasaidia kukua kimapato na hivyo kukuza uchumi. Kwa kukua kwa kipato chao Benki itaongeza idadi ya watu wanaotakiwa kuwa wateja wao hapo baadae.

Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo nchini Tanzania, Ruth Zaipuna, amesema kwamba ripoti hiyo imeonesha mchango wa benki ukuaji wa kiuchumi na hasa sekta binafsi ambayo ndio inatoa wateja.

Alisema benki hiyo itaendelea kufanya juhudi za kuimarisha ushirikiano wake na mataifa ya Afrika Mashariki kupitia bidhaa zake mbalimbali.

...

Monday, March 19, 2018

Shindano la MO Margarine Star kutoa zawadi ya mil 4.2 kwa wanafunzi 10 nchini


Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) imeandaa shindano la kuimba wimbo wa MO Margarine kwa wanafunzi wa elimu ya msingi na sekondali, linalokwenda kwa jina la ‘MO Margarine Star’.
Akizungumza kuhusu shindano hilo, Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Fatema Dewji ametoa masharti ya shindano hilo, kwamba kabla ya mwanafunzi kushiriki shindano hilo anatakiwa apate ridhaa kutoka kwa wazazi ama walezi wake.
Ameeleza kuwa, ili kushiriki shindano hilo, mwanafunzi anatakiwa ajirekodi video akiimba wimbo huo, na kuposti katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram au Facebook kisha kuishirikisha akaunti ya METL inayopatikana na kuweka hashtag ya #MoMargarineStar.
Dewji alisema zawadi kwa washindi ni Sh. 700,000 kwa mshindi wa kwanza, Sh. 600,000 kwa mshindi wa pili, Sh. 500,000 kwa mshindi wa tatu na kuanzia mshindi wa nne hadi 10 watapewa Sh. 400,000 kwa kila mmoja.

PWANI WAPOKEA MBEGU BORA ZA MAHINDI WEMA 2109

 Ofisa mradi wa Mbegu za Mahindi yanayostahimili  Ukame ya Wema 2109  kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kupitia Jukwaa na Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Bestina Daniel, akizungumza wakati wa uzinduzi wa shamba darasa la mbegu hiyo katika Kijiji cha Kilemela kilichopo Kata ya Kerege wilayani Bagamoyo jana. W a pili kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga na hao wengine ni viongozi mbalimbali katika wilaya hiyo.
 Ofisa Kilimo wa Mkoa wa Pwani, Kapilima George akizungumza.
 Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, akitoa hutuba yake.
 Mkurugenzi wa Fedha wa Fedha na Utawala wa COSTECH,Shabani Hussein (kulia), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga  mbegu hizo kabla ya kuzindua shamba darasa. Katika ni Ofisa mradi wa Mbegu za Mahindi yanayostahimili  Ukame ya Wema 2109  kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kupitia Jukwaa na Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Bestina Daniel.
 Mwakilishi wa Kikundi cha Kikuki Malengo Group kutoka Kitongoji cha Amani, Othman Said Ally akikabidhiwa mbegu. Wa pili kulia ni Mtafiti  Kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga mkoani Morogoro, Nikidadi Hamidu.
 Mkulima Julius Maina (kushoto), kutoka Kitongoji cha Zinga akikabidhiwa mbegu.
 Mkulima Anaseli Macha kutoka Kijiji cha Kongo Kaya ya Yombo akikabidhiwa mbegu.
 Mkulima Ahazi Mwasibata akikabidhiwa mbegu.
 Hapa wakielekezwa namna ya upandaji wa mbegu hiyo.
  Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, akizundua shamba darasa hilo kwa kupanda mbegu.
 Ofisa Kilimo wa Mkoa wa Pwani, Kapilima George na Ofisa Kilimo Ushirika na Umwagiliaji wa Wilaya ya Bagamoyo, Mary Kisimbo wakipanda mbegu hiyo.
Mbegu hiyo ikipangwa katika shamba darasa eneo la Zinga.

Na Dotto Mwaibale, Bagamoyo

MKOA wa Pwani umepokea mbegu bora ya mahindi aina ya Wema kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kupitia Jukwaa na Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB) kwa ajili ya kupandwa kwenye mashamba darasa mkoani humo.

Akizungumza wakati akipokea mbegu hiyo wakati wa uzinduzi wa shamba darasa uliofanyika jana katika Kijiji cha Kilemela Kata ya Kerege wilayani Bagamoyo Mkuu wa wilaya hiyo Majid Mwanga alisema mbegu hiyo itasaidia kuondoa changamoto ya kupata mbegu bora kwa wakulima wilayani mwake.

"Niwashukuru wenzetu wa COSTECH na OFAB kwa kutukumbuka kwa kuendesha program hii ya kugawa mbegu bora ya mahindi katika mkoa wetu hususan kwenye wilaya yangu ya Bagamoyo" alisema Mwanga.

Alisema mradi huo utasaidia kuongeza ari ya kilimo cha mahindi kwenye wilaya hiyo na kuunga mkono jitihada za Rais Dk.John Magufuli za kuhimiza kufanya kazi kwa bidii na kuanzisha viwanda hapa nchini.

Aliwaomba wakulima hasa kwa wanavikundi waliopata mbegu hizo kuhakikisha wanayatunza mashamba darasa hayo kwa manufaa ya wakulima wote wa wilaya hiyo.

Ofisa Kilimo wa Mkoa wa Pwani Kapilima George alisema mbegu hizo zitaongeza mazao ya mahindi kwani licha ya kutumia mbegu zingine mkoa huo kwa mwaka jana ulipata tani 110.
  

Akizungumza kwa niaba ya  Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH wakati wa kukabidhi mbegu hizo, Mkurugenzi wa Fedha wa Fedha na Utawala wa COSTECH, Shabani Hussein alisema kazi kubwa ya COSTECH ni kuishauri serikali katika masuala yote yanayohusu  Sayansi na Teknolojia na kusimamia tafiti zote za kisayansi katika maeneo mbalimbali na kilimo na kuhakikisha zinawafikia walengwa.

Alisema mbegu hizo walizozikabidhi zimefanyiwa utafiti na zitapandwa katika mashamba darasa na baadae kusambazwa kwa wakulima wengine ili kuondoa changamoto ya kukosekana kwa mbegu bora kutokana na wakulima kukabiliwa na mbegu ambazo zilikuwa hazina ubora.

Mtafiti  Kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga mkoani Morogoro, Nikidadi Hamidu alisema iwapo mkulima atafuata ushauri wa upandaji wa mbegu hiyo ya Wema 2109 katika ekari moja atapata magunia 35 tofauti na mbegu nyingine ambapo wanapata chini ya hapo.

Ofisa mradi huo kutoka COSTECH, Bestina Daniel alisema kwa mkoa huo wametoa mbegu kilo 58 kwa ajili ya mashamba darasa katika wilaya ya Bagamoyo na Chalinze ambapo kwa wakulima mmoja mmoja wametoa kilo 42 pamoja na mbolea ya kupandia.



Saturday, March 17, 2018

GARI LAGONGA WATOTO KUIKWEPA BODABODA GONGO LA MBOTO

 Wasamaria wema wakiwa wamewabeba watoto waliogongwa na gari la mizigo katika makutano ya Barabara ya Nyerere na Ulongoni, eneo la Kituo Kipya, Gongo la Mboto, Dar es Salaam leo.

Na Richard Mwaikenda, GOMS

WATOTO wawili wamegongwa na gari la mizigo  katika ajali iliyotokea mchana wa leo 
katika makutano ya Barabara ya Nyerere na Ulongoni, Gongo la Mboto (Goms), Dar es Salaam.

Watoto  hao wawili ndugu wa kike na wa kiume wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka minne na mitano walipatwa na mkasa huo muda mfupi baada ya mama yao kuwaacha pembezoni mwa barabara.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wanasema ajali hiyo ilitokea wakati gari  gari namba T 324 PTM lililokuwa kwenye mwendo kasi kuikwepa bodaboda iliyokuwa iliyokatiza ghafla mbele yake, ndipo likapoteza mwelekeo na kuwagonga watoto hao.

Gari hilo ambalo dereva alikimbia baada ya ajali kuogopa kipigo, liliwagonga watoto hao na kuingia kwenye mtaro, lakini kama siyo mtaro lingeingia kwenye nyumba na kusababisha maafa zaidi.Mwendesha bodaboda naye alikimbia kuogopa kipigo.

Watu wengine wakiwemo waendesha bodaboda wanaoegesha kusubiri abiria katika kona hiyo ilipo transfoma, walinusurika kwani wengi wao hawakuwepo na baadhi yao walikimbia baada kuliona gari hilo limekosa mwelekeo.

Wanasema kuwa mama mzazi wa watoto hao ambaye hakuwa mbali sana na eneo la ajali aposikia mkasa huo hakuamini na kilichofuata aliishiwa nguvu na kuanguka chini.

Baadhi ya wasamaria wema waliharakisha kuwachukua watoto hao waliokuwa kwenye hali mbaya na kuwaingiza kwenye Bajaji tayari kuwakimbiza hospitali kwa matibabu. 

Ajabu iliyotokea ni kwamba baadhi ya waendesha Bajaji walikataa katakata kuwapeleka watoto hao Hospitali.

 Watoto waliojeruhiwa wakiwa chini baada ya kuwaokoa chini ya gari kwenye mtaro

 Watoto majeruhi wakiingwa kwenye moja ya bajaji kuwawahisha hospitali, lakini hata hivyo mwendesha bajaji hiyo alikataa kuwapeleka na kuwaamuru wawashushe. IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG;0715264202,0754264203,
 Wakihamia kwenye moja ya Bajaji kuomba msaada huo
 Wakiwaingiza kwenye Bajaji ambayo walikubaliwa
 Mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo akilia kwa uchungu baada ya kuwaona watoto hao
 Wakiangalia ajali hiyo
 Gari hilo nusura liingie kwenye maduka yaliyopo eneo hilo, kilichozuia ni mtaro wa maji taka,

 Trafiki akiangalia ajali hiyo

 Breakdown ikiandaliwa kulivuta gari. Hata hivyo lilishindwa
Gari hilo likivutwa na gari la taka

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...