Friday, September 15, 2017

RC SHIGELA AFUNGUA MKUTANO MKUU WA UMOJA WA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA

Mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigela leo Ijumaa Septemba 15,2017 amefungua mkutano Mkuu wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (Union of Tanzania Press Clubs- UTPC) mwaka 2017. 

Mkutano huo uliokutanisha viongozi wa Klabu za Waandishi wa Habari kutoka mikoa 27 nchini unafanyika katika ukumbi wa Tanga Beach Resort mkoani Tanga. 
Akizungumza wakati wa kufungua mkutano huo ambao utafanyika kwa muda wa siku mbili (Septemba 15 na 16,2017),Shigela alisema serikali inatambua umuhimu wa vyombo vya habari katika maendeleo ya jamii. 
“Ukitaka maendeleo katika jamii lazima ushirikiane na vyombo vya habari,na hata tunapoelekea katika Tanzania ya viwanda ni vyema vyombo vya habari vihusike”,alieleza. 
Alitumia fursa hiyo kuwataka waandishi wa habari nchini kuzingatia maadili katika kazi yao ya uandishi wa habari huku akiwaasa kujiendeleza kielimu ili kufanya vizuri zaidi katika kazi yao. 
“Vyombo vya habari vinafundisha,vinaelimisha, vinahamasisha, vinakosoa na kufichua maovu na ili kutimiza haya ni vyema mkazingatia maadili yenu, mfanye kazi kwa usawa bila upendeleo lakini pia ni vyema mkawa wazalendo”, aliongeza. 

Kwa Upande wake Rais wa UTPC,Deogratius Nsokolo alisema miongoni mwa changamoto zinazoikabili tasnia ya habari ni uwepo wa sera na sheria zinazobinya uhuru wa vyombo vya habari ikiwemo sheria ya Habari ya habari ambayo baadhi ya vifungu vyake siyo rafiki kwa waandishi wa habari. 

“Tunaiomba serikali ifanye marekebisho katika baadhi ya vifungu kwenye sheria hii ambavyo siyo rafiki kwa vyombo vya habari”, aliongeza Nsokolo. 

Awali akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC, Abubakar Karsan alisema mkutano huo umekutanisha pamoja wadau mbalimbali wa habari nchini na viongozi wa klabu za waandishi wa habari kutoka mikoa 27 ya Tanzania Bara na Zanzibar ukifadhiliwa na SIDA. 

Alisema katika mkutano huo wajumbe wanoshiriki watafanya majadiliano mbalimbali kuhusu masuala mbalimbali yanayowahusu waandishi wa habari.

Mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigela akifungua mkutano mkuu wa UTPC
Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC, Abubakar Karsan akizungumza wakati wa mkutano huo.

Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilakwa akizungumza ukumbini
Rais wa UTPC, Deogratius Nsokolo akitoa hotuba

Makamu wa Rais wa UTPC, Jane Mihanji akizungumza ukumbini.


ENDELEA KUANGALIA MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA 

Saturday, August 19, 2017

NMB yazungumza na wajasiriamali Arusha Dodoma na Kilimanjaro

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Christian Mndeme akizungumza alipokuwa akifungua warsha ya siku mojo ya Klabu ya wafanyabiashara wavBenki ya NMB Mkoa wa Dodoma iliyowajengea uwezo wa kibiashara wafanyabiashara.


Ofisa Mkuu Kitengo cha Mikopo Benki ya NMB, Tom Borghols akizungumza na wafanyabishara wa jiji la Arusha namna ya benki hiyo ilivyosongeza huduma kwao katika mkutano na wajasiriamali toka Klabu ya Biashara ya NMB jijini humo.

Wajasiriamali wa jijini Arusha wakimsikiliza Ofisa Mkuu Kitengo cha Mikopo Benki ya NMB, Tom Borghol wakati akizungumza nao namna ya benki hiyo ilivyosongeza huduma kwao katika mkutano uliofanya. 


Wajasiriamali wa jijini Arusha wakimsikiliza Ofisa Mkuu Kitengo cha Mikopo Benki ya NMB, Tom Borghol wakati akizungumza nao namna ya benki hiyo ilivyosongeza huduma kwao katika mkutano uliofanya. 


Wajasiriamali wa jijini Arusha wakimsikiliza Ofisa Mkuu Kitengo cha Mikopo Benki ya NMB, Tom Borghol wakati akizungumza nao namna ya benki hiyo ilivyosongeza huduma kwao katika mkutano uliofanya. 


Warsha ikiendelea.


Mgeni Rasimi kwenye Washa ya Klabu ya wafanyabiashara wadogowadogo na mawakala wa Benki ya NMB Mkoa wa Kilimanjaro, Sebastian Masanja Katibu tawala msaidizi toka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, akizungumza na washiriki wa warsha hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Kuringe Mjini Moshi.



Mkurugenzi Mkuu wa Mikopo wa Benki ya NMB Tanzania Tom Borghols, akizungumza na washiriki wa Warsha ya Klabu ya wafanyabiashara wadowadogo na mawakala wa NMB Mkoa wa Kilimanjaro, warsha hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Kuringe Holl Mjini Moshi.


Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kati, Straton Chilongola akitoa taarifa ya lengo la Benki ya NMB kuwakutanisha wafanyabiashara Mkoa wa Dodoma kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua warsha hiyo.

Baadhi ya wafanyabishara wa jiji la Arusha wakiwa katika mkutano huo.

UVCCM YALAANI UBAGUZI MISIKITINI PEMBA

Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja Wa Vijana wa Chama Cha Mpinduzi UVCCM Ndg Shaka Hamdu Shaka akizungumzia kadhia ya kuzuiwa kuswali waumini wa dini ya kiislamu ambao ni wanachama cha chama cha mapinduzi ccm. (Picha Na Fahad Siraj)


Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja Wa Vijana wa Chama Cha Mpinduzi UVCCM Ndg Shaka Hamdu Shaka akisikiliza taarifa ya kadhia ya kuzuiwa kuswali waumini wa dini ya kiislamu ambao ni wanachama cha chama cha mapinduzi ccm. (Picha Na Fahad Siraj)


Wanachama wakimlaki Kaimu katibu mkuu mara baada ya kuwasili  kuzungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake katika mkutano wa ndani uliofanyika katika ukumbi wa Jamhuri Wilayani Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba.


Na Mathias Canal, Kaskazini Pemba

UMOJA Wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi UVCCM umelaani vikali ubaguzi uliofanywa na baadhi ya Wanachama wasikuwa CCM kwa kuwazuia wanachama wa CCM kuswali pomoja katika misikiti kwenye baadhi ya maeneo Mbalimbali visiwani Pemba.

Umoja huo umesema kuwa kuzuia watu kuswali kisa itikadi za dini zao ni dhambi kwa Mwenyezi Mungu kwani kufanya hivyo ni kupiga amri ya Mwenyezi Mungu anayetoa onyo Kali katika Quran kwa wale wanaothubutu kuwazuia waini wengine kuswali.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja Wa Vijana wa Chama Cha Mpinduzi UVCCM Ndg Shaka Hamdu Shaka Wakati akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake Wakati alipotembelea Msikiti wa Masjid Lmuhajiriina uliopo Eneo la Kiungoni Kimango Wilayani Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema kuwa Imani ya dini yoyote nchini haibagui wala kuchagua watu kuswali kutokana na Itikadi zao za kisiasa ama kikabila kwani dini Ni ibada ya Imani kwa kila mwananchi.

Shaka Alisema kuzuia watu kuabudu Ni makosa kwa mujibu wa taratibu za nchi lakini pia ni Dhambi kwa Mwenyezi Mungu kwani hakuna maandiko yanazuia watu kushiriki katika ibada.

Mnamo Mwaka Mwaka 2016 baada ya kura ya marejeo kikundo Cha watu wachache katika baadhi ya maeneo walianza kuwashawishi Wananchi kususia kuswali na Wanachama wanaotokana na CCM ambapo kwa kiasi kikubwa waliwaunga mkono Jambo lililopelekea waumini was kiislamu watokanao na CCM kuanza kusali majumbani mwao.

WANAVIJIJI IKUNGI WAENDELEA KUNUFAIKA NA MIRADI YA MAENDELEO

Mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Mhe.Miraji Mtaturu (aliyesimama) amezindua awamu ya pili ya mradi wa kuwajengea wananchi uwezo ili kuibua na kuendeleza miradi ya maendeleo katika vijiji vyao wilayani humo.

Katika uzinduzi huo, Mhe.Mtaturu alilipongeza shirika la HAPA kwa kusimamia vyema awamu ya kwanza ya mradi huo na hivyo kufanikisha kupata ufadhiri wa awamu ya pili ya mradi ambapo Vijiji 15 wilayani Ikungi vitanufaika.

Mhe.Mtaturu aliwata wasimamizi wa mradi huo kuendelea kusimamia vyema shughuli za mradi huo jambo ambalo litasaidia upatikanaji wa miradi mingine kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa wilaya ya Ikungi.

Mkurugenzi wa shirika la HAPA, Makyao Noel alisema Vijiji 10 wilayni Ikungi vilifikiwa katika awamu ya kwanza ya mradi huo na hivyo kusaidia wananchi kuibua miradi 26 ya maendeleo na kwamba miradi miradi 12 ilikuwa ya maji, Zahanati, Vituo vya Afya, barabara pamoja na nyumba za watumishi na kwamba awamu ya pili ya mradi huo itavifikia Vijiji 15 wilayani Ikungi.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi, akitoa neno la shukurani kwenye uzinduzi huo uliokwenda sambamba na kujadili mafanikio na changamoto za mradi wa awamu ya kwanza ili kusaidia uboreshaji kwenye utekelezaji wa mradi wa pili utakaodumu kwa miezi sita kuanzia mwezi huu.

Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi, akitoa salamu zake kwenye uzinduzi huo.

Aliyesimama ni Mkurugenzi wa shirika la HAPA, Makyao Noel alisema, akitoa ufafanuzi kwenye uzinduzi huo.

Viongozi mbalimbali meza kuu.

Wawezeshaji wa mradi.

Viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi wakiwemo madiwani wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi huo.

Watendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi huo.

DC IKUNGI AZUNGUMZIA MICHUANO YA "IKUNGI ELIMU CUP"

Mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Mhe.Miraji Mtaturu ametoa ufafanuzi kuhusiana na ligi ya "Ikungi Elimu Cup 2017" itakayozinduliwa kesho Agosti 19,2017 katika uwanja wa shule ya sekondari Ikungi wilayani humo.

Mhe.Mtaturu kaeleza sababu za kuanzishwa kwa ligi hiyo na namna itakavyosaidia kuhamasisha wananchi pamoja na wadau mbalimbali wa elimu katika kutatua changamoto za elimu wilayani Ikungi ikiwemo ujenzi wa madarasa, maabara pamoja na nyumba za waalimu kupitia mfuko wa elimu Ikungi ambapo yeye ni mlezi wa mfuko huo.
BMG Habari

NEW SONG: Hear Our Cry - Varkeize Motema Feat. Larry SingLive and Daisy Nyokabi

This is a prayer for our beloved country Kenya and a call to all Kenyans to unite together. While many may have varied ways of championing for peace love and unity, this is my little contribution to this cause...

Below is youtube link to the video of the song.

Wednesday, July 5, 2017

Mkurugenzi Taasisi ya Doris Mollel Azinduwa Duka la Kadi

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa tawi jipya la Kampuni ya 'R plus event cards', Mwenge Sokoni wauzaji wa kadi mbalimbali na maua ya maharusi jumla na rejareja jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya 'R' plus event cards', Bi. Rehema Moses na Mkurugenzi Mkuu, Raimond Njuu (kushoto) wakishuhudia.


Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel (katikati) akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya 'R plus event cards', Raimond Njuu (kushoto) mara baada ya kuzindua tawi jipya la Kampuni ya 'R' Plus Events Cards, Mwenge Sokoni wauzaji wa kadi mbalimbali na maua ya maharusi jumla na rejareja jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya 'R' Plus Events Cards, Bi. Rehema Moses akishuhudia.


Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya 'R' Plus Events Cards, Bi. Rehema Moses (kushoto) akimuonesha Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel (kulia) sehemu ya bidhaa zinazouzwa na duka hilo mara baada ya kuzinduliwa. Kampuni ya 'R' Plus Events Cards, wauzaji wa kadi mbalimbali na maua ya maharusi jumla na rejareja imezinduwa tawi jipya Mwenge Sokoni jijini Dar es Salaam.


Hapa ikikatwa keki ya pongezi na viongozi wa Kampuni ya Plus Events Cards.


Picha ya pamoja ya wageni waalikwa baada ya uzinduzi.


MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Bi. Doris Mollel amezinduwa tawi jipya la duka la kadi la Kampuni ya 'R' Plus Events Cards' Mwenge, Sokoni Jijini Dar es Salaam huku akiwataka wajasiliamali wadogo na wakubwa wauzaji wa bidhaa hizo kujitokeza kuchangamkia fursa hiyo ili wajipatie kipato. Bi. Mollel ametoa kauli hiyo alipokuwa akizinduwa tawi hilo, linalofunguliwa kusogeza huduma za uuzaji kadi za kisasa jumla na rejareja kwa wananchi eneo hilo.

 Pamoja na hayo, Bi. Doris Mollel aliwashauri wananchi kupenda kununua bidhaa halisi na kuachana na bidhaa feki kwani zimekuwa na madhara huku zikilikoseshea taifa mapato. Alisema bidhaa nyingi feki haziingii kwa utaratibu rasmi nchini hivyo licha ya madhara kwa watumiaji zimekuwa zikilikosesha taifa mapato.

 "...Nashauri Watanzania wenzangu tupende kununua bidhaa halisi zinazoendana na thamani ya fedha tunazotoa. Uzuri sasa hivi wauzaji wengine wamekuwa wawazi wanakwambia hii ni bei rahisi kwa kuwa ni feki na hii ndio bidhaa halisi...tujenge utamaduni wa kutumia bidhaa bora na halisi kwa manufaa yetu na taifa," alisisitiza Bi. Doris Mollel.

 Aidha aliipongeza kampuni ya Plus Events Cards wauzaji wa kadi na maua ya maharusi kwa kusogeza huduma zake eneo la Mwenge na kutoa fursa kwa wajasiriamali kuwatembelea kwa ajili ya kusambaza bidhaa hizo Dar es Salaam na hata mikoani. Aliongeza kuwa hatua hiyo si tu imesogeza huduma kwa wahitaji bali imetoa fursa kwa wajasiriamali wadogo kupata bidhaa za kadi kirahisi na kuzisambaza kwa wahitaji.

  Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na viongozi wa Kampuni ya R Plus Events Cards mara baada ya uzinduzi. Wa kwanza kushoto na kulia ni baadhi ya wafanyakazi wa duka hilo tawi la Mwenge Sokoni.


Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya R Plus Events Cards, Bi. Rehema Moses (kushoto) akimlisha keki ya pongezi Mkurugenzi Mkuu, Raimond Njuu (kushoto) mara baada ya uzinduzi.


Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya R Plus Events Cards, Raimond Njuu (kulia) akiwashukuru baadhi ya wageni waalikwa mara baada ya uzinduzi wa tawi lao lililopo Mwenge Sokoni wauzaji wa kadi mbalimbali na maua ya maharusi jumla na rejareja jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya R Plus Events Cards, Bi. Rehema Moses ameiomba Serikali kujenga mazingira ya ulipaji kodi na malipo anuai ya vibali vya biashara kufanyika eneo moja ili kupunguza urasimu ambao wamekuwa wakiupata wafanyabiashara wanapoitaji kulipia tozo hizo.

Mkurugenzi huyo Mtendaji alitoa kauli hiyo kwenye uzinduzi wa tawi jipya la uuzaji kadi jumla na rejareja kwa ajili ya matukio mbalimbali ya sherehe eneo la Mwenge, Sokoni jijini Dar es Salaam. Bi. Moses alisema wapo wafanyabiashara waadilifu ambao wanajua umuhimu wa kulipia tozo mbalimbali na vibali vya biashara wanazozifanya lakini baadhi wamekuwa wakikwazwa na urasimu uliopo katika ufuatiliaji wa vibali hivyo na mtawanyiko wa ofisi anuai za kufanyia malipo, jambo ambalo linachangia kujikuta wanashindwa kulipia kwa wakati.

 Mfanyabiashara huyo mwanamama na Mtanzania wa kwanza kusambaza bidhaa hizo za kisasa aliiomba Serikali kuangalia uwezekano wa vibali vyote na malipo kuwa yakifanyika eneo moja ili kumrahisishia mfanyabiashara kukamilisha vibali husika kwa wakati, na kumpunguzia mfanyabiashara vikwazo ambavyo wakati mwingine vimekuwa vikimpotezea muda mwingi katika ufuatiliaji.

 Aidha alivishauri vyombo vya kudhibiti ubora wa bidhaa kuongeza nguvu ili kudhibiti baadhi ya wafanyabiashara ambao wamekuwa wakichapisha kadi feki nchini na kuwalaghai watanzania kuwa ni halisi, jamboa ambalo linawaharibia wafanyabiashara wanaosambaza bidhaa halisi. Alisema kampuni yake ambayo imekuwa ikisambaza kadi za kisasa za matukio mbalimbali ya sherehe jumla na rejareja kutoka nchini China ipo tayari kuwasaidia wajasiliamali waaminifu kutoka popote nchini kufanya biashara hiyo bila udanganyifu ili kumpatia mlaji wa mwisho bidhaa halisi kwa bei nzuri.


Kulia ni mfanyakazi wa Kampuni ya Plus Events Cards, akimuonesha mmoja wa wateja baadhi ya bidhaa mara baada ya uzinduzi huo.


Picha ya pamoja ya wageni waalikwa baada ya uzinduzi.


SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...